Abraham Ntambara
KAMANDA wa Polisi Kanda Maalumu ya
Dar es Salaam Simon Sirro, amesema jeshi hilo lilikuwa sahihi kumuua kijana
aliyetuhumiwa kwa ujambazi wa kutaka kupora fedha zilizokuwa zikisambazwa
katika ATM za tawi la benki ya CRDB Kurasini hivi karibuni.
Kauli hiyo aliitoa jana wakati
akizungumza na waandishi wa habari, alisema jeshi hilo halipo kwa ajili ya
kumuonea mtu hivyo kitendo hicho
kilitokea kwenye tukio na kwamba hakufuatwa nyumbani kwake.
“Kimsingi kama kuna mtu anashaka na
hilo upelelezi upo umefanyika, warudi kwenye eneo la tukio wakaulizie, kama ni
mtu mwema alapoambiwa asimame angefanya hivyo na kunyanyua mikono juu, lakini
hakufanya hivyo bali alikuwa akimfuata askari,”
“Sasa ulitaka askari afanye nini
akimbie?, waende pale wakaulize, watu wapo tumewauliza na wametueleza mambo
ambayo amekuwa akifanya yule kijana, sisi hatupo kumuonea mtu, ni kutenda haki,
ukiingia kwenye laini yetu ya uhalifu tutakushughulikia kwa mujibu wa sheria,”
alisema Sirro.
Aidha alisema amekuwa akiona malalamiko
kwamba kijana huyo alikuwa mwanafunzi mzuri, anafundisha Madrasa pamoja
nakufundisha online ambapo aliwataka wananchi kukumbuka kuwa mazingira ambayo
mauaji yalifanyiak yanafahamiaka kutokana na nikutokana na kwamba kulikuwa na
fedha ambazo zilitaka kuporwa.
Alisema hata kama mtoto wako kama ni
muharifu hawezi kukuambia, aukuwa mwalimu wa madrasa ndiyo huwezi kuwa mharifu
Kamshina Sirro alisisitiza kuwa watu
kusema hakuwa jambazi siyo siyo sahihi kwani suala hilo ni lakiupelelezi na
upelelezi ndiyo unaoweza kulibaini hilo.
Mei 14 mwaka huu Jeshi la Polisi
Kanda Maalumu ya Dar es Salaam katika eneo la Kurasini kwenye jengo la Mako
Makuu ya Uhamiaji lilifanikiwa kumuua kwa risasi mtu aliyesadikiwa kuwa ni
jambazi akijaribu kumnyang’anya silaha askari aliyekuwa akisindikiza gari la
kampuni ya G4S lililokuwa limebeba fedha Tsh. 320,000,00 zilizokuwa
zikisambazwa kwenye ATM za Benki ya CRDB.
Aidha baada ya tukio hilo kuna
taarifa za ndugu na jamaa wamarehemu walijitokeza na kukanusha kuwa ndugu yao
hakuwa jambazi.
mwisho
Comments