Mkurugenzi wa Operesheni na
Teknolojia wa Benki ya Posta Tanzania (TPB) Jema Msuya wa kwanza kulia na Makamu
wa Rais wa Kampuni ya StarTimes nchini Zuhura Hanifu wakikata utepe katika
hafla jana jijini Dar es Salaam ambapo Kampuni ya StarTimes imeingia ubia na
TPB kwa lengo la kuwakopesha wateja televisheni za kidigitali kwa awamu kupitia
mkopo ambao utamwezesha kulipa ndani ya mwaka mmoja kutoka benki hiyo.(PICHA NA
Abraham Ntambara)
Abrahm Ntambara
KAMPUNI ya StarTimes imeingia ubia na
Benki ya Posta Tanzania (TPB) kwa lengo la kuwakopesha wateja televisheni za
kidigitali kwa awamu kupitia mkopo ambao utamwezesha kulipa ndani ya mwaka
mmoja kutoka benki hiyo.
Akizungumza wakati wa hafla ya
kuingia katika ubia huo, Makamu wa Rais wa Kampuni ya StarTimes nchini Zuhura
Hanifu, alisema hiyo ni njia rahisi itakayomsaidia mteja wao kulipia
televisheni yake kwa awamu.
“Wateja wataweza kuipata huduma hii
katika mikoa mitano, Dar es Salaam, Dodoma, Mwanza, Arusha na Mbeya ambapo kuna
matawi ya benki hiyo,” alisema Hanifu.
Meneja Uhusiano wa Kampuni hiyo
Antony Katunzi alisema, “Ushirikiano huu unaashiria wazi mapindizi ambayo benki
na kampuni ya televisheni zinaweza kuleta, kwa kurahisisha ulipaji kwa wateja
wao na jamii kwa ujumla ili kuwezesha kila familia kumiliki luninga ya
kidigitali ya StarTimes,”.
Meneja Masoko wa TPB alisema benki
hiyo imekubaliana na StarTimes kutoa mikopo hiyo midogo kwenye mikoa mitano
amabayo inapata huduma za benki hiyo.
Alisema katia hatua hiyo wateja wasio
wa kampuni hyo wanaweza pia kulipia luninga hizo kwa awamu kupitia matawi yote
ya TPB, waishio mijini na vijijini wataweza kupata luninga kwa urahisi
kulingana na mahitaji yao.
Naye Mkurugenzi wa Operesheni na
Teknolojia wa TPB Jema Msuya alisema kuwa kwa awamu ya kwanza wataanza kutoa
huduma ya mikopo hiyo kwa wafanyakazi wa Taasisi za serikali pekee.
Aidha alieleza kuwa watakao hitaji
mikopo hiyo wakifika benki watashughulikiwa nadani ya siku tatu na kisha kupata
mikopo hiyo ambapo wataenda katika madoka ya StarTimes na kupatiwa luninga.
Luninga hizo za kidigitali zimetolewa
katika matoleo mbalimbali ili kuendana na wateja kulingana na mahitaji na uwezo
wao. Zilitajwa luninga hizo kuwa ni inchi 24 kwa sh.45000, inchi 32 kwa sh.
64000 na inchi 40 kwa sh.99000.
mwisho
Comments