Ofisa Elimu Maalum Wilaya Ilala, Salehe Msechu wa pili kutoka kulia akionesha kitabu cha nukta nundu, katika hafla ya kukabidhi vitabu 20 vya nukta nundu kwa ajili ya wanafunzi wasioona katika Shule ya Uhuru Mchanganyiko jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mjumbe wa Baraza la Uongozi la Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Madeline Kimei, akifuatiwa na Mtendaji Mkuu wa Chama cha Wasiona Tanzania, Jonas Lubago na Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Anna Mshana. (PICHA NA SULEIMAN MSUYA)
Suleiman Msuya
JUKWAA la Haki na Usalama linatarajia kugawa vitabu 7,000 ambavyo vimebeba ujumbe kuhusu mambo 101 mwananchi anapaswa kuyajua kuhusu polisi huku vitabu 300 vikilenga watu wenye mahitaji maalum.
Hayo
yamesemwa na Mjumbe wa Baraza la Uongozi la Chama cha Wanasheria Tanganyika
(TLS), Madeline Kimei wakati akizindua na kukabidhi vitabu 20 vya nukta nundu kwa
Shule ya Msingi Uhuru Mchanganyiko iliyopo Ilala jijini Dar es Salaam jana.
Alisema
TLS imejipanga kugawa vitabu hivyo ambayo vitasaidia jamii ambayo imekuwa
ikikutana na changamoto mbalimbali wakati ikikutana na polisi.
Kimei
alisema TLS kwa kushirikiana na Jukwaa la Haki na Usalama imeweza kuandaa
machapisho manne yanayohusu polisi ambapo mawili ni nyaraka za majadiliano
ambayo inahusu uhuru wa kioperesheni na uwajibikaji wa jeshi hilo.
Alisema
mengine mawili ni vitabu vya kutoa uelewa kwa wananchi juu ya polisi na mbaraza
ya usalama ya wilaya ambapo mwitikio umekuwa mkubwa.
“Siku
ya leo tuko hapa kwa ajili ya kuzindua toleo la nukta nundu la moja wapo ya
vitabu vilivyochapishwa chini ya mradi huu ambapo kitabu hiki kinaitwa “mambo
101 unayoyahitaji kuyafahamu juu ya polisi lakini unaogopa kuyauliza,” alisema.
Mjumbe
huyo alisema uandaaji wa vitabu vya nukta nundu unagharama kubwa lakini kutokana
na wao kutambua umuhimu wa kundi hilo wamelazimika kuchapisha vitabu 300 kwa
kuanzia katika kundi hilo.
Kimei
alisema kitabu hicho kitaelimisha jamii jinsi jeshi hilo linavyofanya kazi na
ukomo wake wa madaraka hivyo kila pande kutekeleza majukumu yake kwa haki.
Akizungumza
baada ya uzinduzi huo Ofisa Elimu Maalum Wilaya ya Ilala, Salehe Msechu alisema
uamuzi wa Jukwaa la Haki na Usalama ni wa kuungwa mkono na jamii huku
akisisitiza wadau wengine kujitokeza kusaidia.
Msechu
alisema Serikali imejipanga kusaidia kundi la watu maalum hivyo itajitahidi
kutoa vifaa mbalimbali ambavyo vitatumika kwa wanafunzi katika wilaya hiyo.
Mwalimu
Mkuu wa Shule ya Msingi Mchanganyiko, Anna Msechu alisema shule hiyo ina
wanafunzi 69 wasiona hivyo vitabu hivyo vya nukta nundu vitasaidia kuatua
tatizo.
“Hapa
nina wanafunzi 69 ambao watafaidika na vitabu hivi havikidhi hitaji lakini
vitasaidia kwa kiasia fulani tunaomba wadau wengine kujitokeza kusaidia,”
alisema.
Mtendaji
Mkuu wa Chama cha Wasiona Tanzania, Jonas Lubago alisema vitabu vya watu wa
elimu maalum hasa wasiona kwa Tanzania vinapatikana kwa chini ya asilimia mojo
hivyo jitihada zinahitaji ili kukidhi hitaji.
Mwisho
Comments