WAHAMIAJI HARAMU 411 WAKAMATWA BAGAMOYO ,KIPINDI CHA MIEZI SITA ILIYOPITA


Tokeo la picha la MHANDISI NDIKILO PICHA
Mkuu wa Mkoa wa Pwani mhandisi Evarist Ndikilo, akizungumza jambo baada ya kupatiwa taarifa ya kuingia kwa wahamiaji haramu 72, huko Bagamoyo
Tokeo la picha la MKUU WA WILAYA YA BAGAMOYO
Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, alhaj Majid Mwanga akitolea ufafanuzi tatizo la wahamiaji haramu wilayani hapo. (picha na Mwamvua Mwinyi) 

Na Mwamvua Mwinyi, Bagamoyo 

Jeshi la polisi limewakamata wahamiaji haramu 72 raia kutoka nchini Ethiopia kwa kosa la kuingia nchini bila kibali. 

Aidha katika kipindi cha miezi sita,wahamiaji haramu 411 kutoka maeneo mbalimbali,walikamatwa wilayani Bagamoyo.  

Kamanda wa polisi wilaya ya Bagamoyo Adam Maro, alimwambia mkuu wa mkoa wa Pwani, Evarist Ndikilo, kwamba wahamiaji hao walikamatwa usiku wa kuamkia jana .

Alieleza wahamiaji hao walikutwa wakiwa wametelekezwa na mwenyeji wao aliyekuwa akiwasafirisha kutoka Ethiopia kwenda Afrika Kusini kwenye eneo la pembezoni kidogo mwa fukwe ya bahari ya hindi katika kata ya Nianjema. 

Kamanda Maro, alisema matukio ya wahamiaji wanaoingia bila kibali na magendo kupitia Bagamoyo yamekuwa yakitokea mara kwa mara kutokana na njia za panya hasa bahari . 

Nae mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, alhaj Majid Mwanga, alisema tatizo la kuingia kwa wahamiaji haramu katika mwambao wa bahari ya Hindi na kupitia bandari bubu zilizo wilaya hiyo. 

Akizungumza baada ya kupatiwa taarifa hiyo, mkuu wa mkoa wa Pwani, mhandisi Ndikilo, alitoa onyo kwa watu wanaofanya biashara ya kusafirisha wahamiaji haramu . 

Mhandisi Ndikilo, alibainisha wasafirishaji hao waache tabia hiyo mara moja kwani watachukuliwa hatua kali za kisheria.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*