Breaking News: Polisi Dar Waua Watuhumiwa Wawili wa Ujambazi, Mmoja Ajeruhiwa


JESHI LA POLISI Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewaua watu wawili wanaodaiwa kuwa ni majambazi huku mmoja akijeruhiwa na kukimbizwa hospitali kwa matibabu.

Akitoa ripoti ya mafanikio ya Jeshi hilo, Kamanda wa Operesheni, ambaye pia ni Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lucas Mkondya amesema kuwa jeshi hilo pia limefanikiwa kukamata silaha mbili na risasi 5.

“Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar, mnamo 19/06/2017 majira ya saa saa 1:30 jioni maeneo ya Kigogo Luhanga lilifanikiwa kukamata majambazi wawili wakiwa na shotgun na risasi 5 baada ya majibizano ya risasi kati ya majambazi hao.

“Wakiwa katika doria, askari waliona pikipiki mbili za wa zilizobeba watu wawili wawili kila moja, polisi walizifuatilia baada ya kuwatilia shaka watu hao. Watu hao walibaini kuwa wanafuatiliwa kuwa wanafuatiliwa na kuanza kurisha risasi ambapo wawili walijeruhiwa. Baada ya uchunguzi ilibainika ni majambazi waliofanya mauaji maeneo ya Makuburi huku wenzao wawili wakikimbia na pikipiki.

“Katika harakati za kuwapeleka hospitali majambazi waliojeruhiwa, walifariki dunia wakiwa njiani,” Alisema Mkondya.
MSIKIE KAMANDA AKIZUNGUMZA
Tupia Comment Yako, Matusi Hapana

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA