Bunge la Seneti kuchapisha ushahidi unaomshutumu Rais Trump


USA
Image captionRais Trump na James Comey
Kamati ya Bunge la Seneti la masuala ya usalama nchini Marekani imechapisha ushahidi utakaotolewa na mkurugenzi aliyetimuliwa kazi FBI ambaye amesema Rais Trump alimtaka mkurugenzi huyo kuacha kumchunguza mshauri wa zamani wa masuala ya usalama.
James Comey alitoa uchambuzi wa ushaidi wa mazungumzo kati yake na rais Trump aliyofanya naye mara tano wakati Trump alipokuwa akirudia kutaka amsikilize na kumheshimu wakati ambapo Comey anasema alikuwa akifanya kazi zake bila kuegemea upande wowote.
Wakili wa Trump amesema rais Trump anahisi kuna ukweli kwa uthibitisho kuwa yeye mwenyewe binafsi hakuwa akichunguzwa kwa timu yake ya kampeni zake kuhusishwa na Urusi.
Maafisa wawili wanaohusika na usalama,Mike Rogers na Dan Coats wamewaambia maseneta kuwa hawakuwahi kulazimishwa kufanya jambo lolote ambalo liko kinyume na sheria.

Mada zinazohusiana

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*