Mashabiki wa Yanga Waichoma Moto Jezi ya Niyonzima


Mashabiki wa Yanga wameonyesha hasira zao kwa kuchoma moto jezi ya Haruna Niyonzima.
Mashabiki hao wa Yanga wameonyesha kuchukizwa na uamuzi wa Niyonzima kutosaini mkataba Yanga baada ya kushindwana na uongozi wa klabu hiyo.
Niyonzima ameamua kwenda Simba baada ya uongozi wa Yanga kushindwa kuongeza mkataba kutokana na kutokuwa na dau la kutosha.
Jana mchana, uongozi wa Yanga kupitia katibu wake mkuu, Charles Boniface Mkwasa ulitangaza kumuacha Niyonzima kwenda anakohitaji baada ya mkataba wake kwisha.
Yanga imesisitiza, imempa Niyonzima mkono wa kheri kwa kuwa haina uwezo wa kumsajiri tena.
Mashabiki hao wanaoelezwa kuwa ni wa Dar es Salaam, wamesikika wakipongezana kutokana na uamuzi wao wa kushoma jezi hizo namba 8 ambayo ilikuwa ikivaliwa na Niyonzima aliyeichezea Yanga kwa miaka sita.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*