MWENYEKITI WA BUNGE AONGOZA MAZISHI YA MAMA WA MTEMVU


Enzi ya uhai wa Sitti Mtemvu
Mazishi ya Sitti Mtemvu,  mama wa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Temeke, Abbas Mtemvu yaliyofanyika Dar es Salaam,  Juni 2, 2017 katika makaburi ya  Kinondoni ya kiongozwa na Mwenyekiti wa Bunge la Tanzania Mh, Azzan Zungu na kuhudhuriwa na  viongozi mbalimbali akiwepo Wananchi, Mkuu wa Majeshi Mstaafu Tanzania, Davis Mwamunyange , Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Felix Lyaniva, Wabunge wastaafu, Bi Sophia Simba, Mh, Adam Malima, Mh, Idd Azani, Mh, Vita Kawawa, na viongozi wengine akiwemo,  Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), MNEC wa Wilaya ya Temeke, Phares Magesa , Mbunge, Mariam Kisangi, Naibu Meya wa Kigamboni , Naibu Meya wa Temeke, Meneja wa DDC, Meneja wa Dawasco, Mh, Diwani wa Temeke, Kinondoni, Ilala, Mwenyekiti wa Vijana CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Omary Matulanga na  Mkuu wa Idara ya Utawala UVCCM Taifa,  Omary Mwanangwalu. (PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA) Mmiliki wa ujijirahaa blog

Gari maalum lililoandaliwa na familia  lakubeba mwili wa marehemu uliokuwa umehifadhiwa Hospitali ya Lugalo 
Mtoto wa Marehemu Amina Mtemvu (katikati) akisaidiwa na mama mtemvu kushoto na kulia Hellen Mwilima  baada ya kuutambua mwili wakati walipofika katika Hospitali ya Lugalo kuuchukuwa mwili wa marehemu kuelekea nyumbani kwa taratibu za mazishi
Mwili wa marehemu Sitti Mtemvu ukiingizwa katika gari maalumu ukitokea Hospitali ya Lugalo kuelekea nyumbani kwa taratibu za mazishi
Mwili wa Marehemu Sitti Mtemvu ukishushwa nyumbani 
Wajukuu wa Marehemu Sitti Mtemvu wakiwa wamebeba picha ya marehemu
Mwili wa marehemu Sitti Mtemvu ukiwasili nyumbani ukipokelewa na waombolezaji ukitokea Hospitali ya Lugalo ukiingizwa ndani kabla ya kutowa heshima za mwisho
Mchungaji Huduma Neno lililopo Mbagala Mgeninani, Yohana Msumule akiongosa kwa Ibada fupi baada ya mwili kuwasili nyumbani  
Familia ikiwa katika huzuni
Wadogo wa Mtemvu na Mh, Mtemvu wakiwa katika majonzi
Mdogo wa Marehem Hamisi Mtemvu akitowa heshima za mwisho kabla ya kwenda makaburini 
Mdogo wa Marehem Hamisi Mtemvu akizungumza jambo na ndugu na familia yake baada ya yeye kutowa heshima za mwishi 




Waombolezaji kwa kushirikiana na familia wakiuandaa mwili kwa kuuweka sehemu maalum ya kuagia 
Sitti Mtemvu (kushoto) akizungumza na mama yake mama Mtemvu





Waombolezaji wakiwa wameubeba Mwili wa marehemu Sitti Mtemvu mara baada ya kukiwazili katika makaburi ya Kinondoni Jijini  Dar es Salaam

Mchungaji Huduma Neno lililopo Mbagala Mgeninani, Yohana Msumule akiongosa kwa Ibada fupi baada ya mwili kuwasili nyumbani  
Waombolezaji
  Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya mkoa ya Temeke, Dk. Amaani  Malima (aliye simama kushoto)
Mchungaji Huduma ya Maombezi Mbezi Beach Dar es Salaam, Atilio Komba, ambaye ni Mjukuu wa Marehemu Moris Nyunyusa (kulia) akitowa mahubilr katika makaburi ya Kinondoni kabla ya mazishi ya mama wa Mh, Abbas Mtemvu




Amina Mtemvu akitowa heshima za mwisho kwa kuweka udongo katika kabuli la mama yake

Aliyekuwa Mbunge wa Jibo la Temeke Mh, Abbas Mtemvu akitowa heshima za mwisho akiweka udongo katika kaburi la mama yake Juni 2, 2017 katika makaburi ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam
Mtoto wa marehemu Sitti Mtemvu,  Herry Mtemvu akitowa heshima za mwisho akiweka udongo katika kaburi la mama yake Juni 2, 2017 katika makaburi ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam

Mh, Adam Malima  akitowa heshima za mwisho kwa kuweka udongo

 Mariam Mtemvu (kushoto)  akitowa heshima za mwisho kwakuweka udongo

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), MNEC wa Wilaya ya Temeke, Phares Magesa akitowa heshima za misho

Kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Sharik Choughule (aliyevaa suti nyeusi) akiweka udongo katika kaburi la mama 






Mkuu wa Majeshi Mstaafu Tanzania, Davis Mwamunyange, (kulia) akimpa pole aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Temeke, Abbas Mtemvu 







Mh, Mtemvu na mkewe wakiweka shada la maua katika kaburi la mama yao


Mh, Malima akiweka shada la maua na mkewe  katika kaburi la mama wa Mtemvu


















Na Kamisi Mussa

Sitti Mtemvu ambaye alikuwa Mama  wa aliyekuwa Mbunge wa Temeke, Abbas Mtemvu amezikwa Juni 2, 2017 katika Makaburi ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam, ambapo Bi, Sitti Mtemvu  alipata Elimuya yake ya msingi katika Shule ya Jamiatul Islamiya iliyopo Mtaa wa Lumumba na Aggrey wakati huo ukiitwa New street na Stanley street.

 Marehemu, Sitti alifunga ndoa na Hayati Zuberi Mtemvu 
mnamo miaka ya mwanzoni ya 1950, kipindi ambacho wote walijihusisha na shughuli za kisiasa za kudai Uhuru wa Tanganyika, 

Wakati mumewe alikuwa Katibu wa kwanza wa Chama Cha TANU chini ya Hayati Mwalimu  Nyerere, ambapo  marehemu  Sitti  alijishughulisha na kuwahudumia wanasiasa hao wakati wapo kwenye mikutano ya siri iliyokuwa inafanyika nyumbani kwao

 Kipindi hicho harakati za ukombozi zilikuwa zinafanywa kwa siri majumbani, ambapo nyumba ya 
baba yake Marehemu Sitti iliyokuwa wanaishi ilitumika sana.

Harakati hizo ziliwashirikisha wakinamama, Maria 
Nyerere, Sofia Kawawa, Bi Titi Mohamed na wengine, Marehemu pia alijiunga na vijana wengine kwenye mafunzo mbalimbali yaliyokuwa yanafanyika huko Arnatoglo Hall ambapo kulikuwa na mkusanyiko wa vijana wasomi waliojipanga kutawala Nchi yao.

Hapo ndipo chimbuko la  Chama cha TAA na hatimaye TANU ilipoanzishwa , vilevile alijiunga na Elimu ya 
watu wazima na kusoma Lugha ya Kiingereza. Mnamo miaka hiyo marehemu alisafiri mikoa 
mbalimbali kuanza harakati za kudai uhuru dhidi mkoloni,

Marehemu aliwahi kuwa kiongozi wa ngazi 
mbalimbali katika umoja wa wanawake wa Tanganyika wakati huo na hata na baada ya 
Muungano wa Tanzania. marehemu alifanya kazi Tanzania Cigarette Company mnamo miaka ya 1965 na 1973 wakati huo BAT na Bank of Tanzania na kustaafu mwaka 1973.

 Baada ya kustaafu marehemu alijishughulisha na biashara mbalimbali ikiwemo ufugaji wa kuku mnamo mwaka 1987 marehemu alihamia nchini Ivory Coast Abidjan na kufanya biashara ya kuendesha mgahawa 
wa chakula kwa kushirikiana na familia yake.

Marehemu alilazimika kurudi nchni baada ya 
machafuko ya kisiasa yaliyotokea nchini humo mnamo mwaka 1990.Marehemu alifariki mnamo Mei 30, 2017usiku kwa maradhi yaliyosababishwa na tatizo la sukarina umuri mkubwa 

mwisho.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

ALLY KAMWE AZIMIA KWA MKAPA.

RAIS SAMIA KUZINDUA MKUTANO MKUU WA 79 WA BARAZA LA MICHEZO YA MAJESHI DUNIANI

MIGINGO KISIWA KIDOGO ZAIDI AFRIKA KILICHOGOMBEWA NA UGANDA, KENYA