RAIS Mstaafu wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi, mapema leo Jumatatu amewaongoza waumini wa Kiislamu katika kusherehekea Sikukuu ya Eid El Fitr, katika swala ya Eid El Fitr iliyofanyika kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na waumini mara baada ya swala hiyo, mzee Mwinyi aliwataka Waislamu wote nchini kusherehekea sikukuu hiyo kwa kufanya matendo mema ya kumpendeza Mwenyezi Mungu.
“Waumini wa Dini ya Kiislam muendeleze ushirikiano,umoja na mshikamano na madhehebu mengine ya dini nchini, pia mwendeleze kudumisha matendo mema kama mlivyofanya kipindi cha mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani,”alisema.
Comments