Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
Na Richard Mwaikenda
SERIKALI imepiga marufuku uuzaji wa mahindi nje ya nchi na watakaokiuka watachukuliwa hatua kali ikiwemo kutaifisha mahindi na magari yanayosafirisha.
Agizo hilo limetolewa na Wazizri Mkuu, Majaliwa Kassim Majaliwa alipokuwa akihutubia wakati wa swala ya Id el Fitri mjini Moshi leo.
Amesema wameamua kupiga marufuku usafirishaji wa mahindi nje ya nchi, ili kulinda upungufu wa chakula nchini.
Amesema kuwa wengi wa wafanyabiashara wamekuwa wakisafirisha vyakula kwenda nchi jirani, ili hali hapa nchini kuna uhaba wa vyakula. Ameruhusu mfanyabiashara badala ya kusafirisha mahindi asagishe na kusafirisha unga kwa kibali maalumu kutoka kwa mkuu wa mkoa.
Pia ameruhusu kusafirisha chakula kwenda mikoa yenye uhaba wa vyakula hapa nchini, badala ya kupeleka kuuza nje ya nchi.
Pia amemuagiza Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, kumvua cheo askari yeyote atayejihusisha au kuruhusu wafanyabiashara kusafirisha vyakula nje ya nchi.
Na Richard Mwaikenda
SERIKALI imepiga marufuku uuzaji wa mahindi nje ya nchi na watakaokiuka watachukuliwa hatua kali ikiwemo kutaifisha mahindi na magari yanayosafirisha.
Agizo hilo limetolewa na Wazizri Mkuu, Majaliwa Kassim Majaliwa alipokuwa akihutubia wakati wa swala ya Id el Fitri mjini Moshi leo.
Amesema wameamua kupiga marufuku usafirishaji wa mahindi nje ya nchi, ili kulinda upungufu wa chakula nchini.
Amesema kuwa wengi wa wafanyabiashara wamekuwa wakisafirisha vyakula kwenda nchi jirani, ili hali hapa nchini kuna uhaba wa vyakula. Ameruhusu mfanyabiashara badala ya kusafirisha mahindi asagishe na kusafirisha unga kwa kibali maalumu kutoka kwa mkuu wa mkoa.
Pia ameruhusu kusafirisha chakula kwenda mikoa yenye uhaba wa vyakula hapa nchini, badala ya kupeleka kuuza nje ya nchi.
Pia amemuagiza Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, kumvua cheo askari yeyote atayejihusisha au kuruhusu wafanyabiashara kusafirisha vyakula nje ya nchi.
Comments