SIMBA SC YASAJILI WA SITA, STRAIKA LA ZAMBIA MAWINDONI


Na Princess Asia, DAR ES SALAAM
SIMBA SC imetambulisha mchezaji wa sita kusajili, ambaye ni beki Ally Shomary kutoka Mtibwa Sugar ya Morogoro.
Makamu wa Rais wa Simba, Geoffrey Nyange ‘Kaburu’ amemkabidhi jezi ya klabu hiyo Shomary baada ya kusaini mkataba wa miaka miwili kuhamishia shughuli zake Msimbazi kutoka Manungu.
Shomary anaungana na kipa Emanuel Elias Mseja, mabeki Jamal Mwambeleko waliosajiliwa kutoka Mbao FC, Yussuf Mlipili kutoka Toto Africans zote za Mwanza, Shomary Kapombe na mshambuliaji John Bocco kutoka Azam FC. 
Makamu wa Rais wa Simba, Geoffrey Nyange ‘Kaburu’ akimkabidhi jezi beki Shomary baada ya kusaini mkataba wa miaka miwili kutoka Mtibwa Sugar na chini Shomaru akisaini mkataba

Pamoja na hayo, tayari kuna taarifa Simba SC imemsajili kipa namba moja Tanzania, Aishi Manula, huku pia ikiwa mbioni kumrejesha mshambuliaji wake wa zamani, Mganda Emmanuel Okwi kutoka SC Villa ya kwao.
Mshambuliaji wa FC Nkana ya Zambia, Walter Bwalya naye anatajwa kuwa kwenye rada za Wekundu wa Msimbazi.
Simba inafanya usajili wa kishindo, baada ya kufanikiwa kukata tiketi ya kurejea kwenye michuano ya Afrika mwakani kwa mara ya kwanza baada ya mitano.
Wekundu hao wa Msimbazi watashiriki Kombe la Shirikisho Afrika mwakani, kufuatia kutwaa Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), maarufu kama Azam Sports Federation Cup (ASFC) mei 27 mwaka huu kwa kuifunga Mbao FC 2-1 Uwanja wa Jamhuri, Dodoma. 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.