Snura Mushi aeleza chanzo cha ajali mbaya aliyonusurika


Snura Mushi aeleza chanzo cha ajali mbaya aliyonusurika

0
Snura Mushi amekana habari zilizoenea kuhusu chanzo cha ajali mbaya aliyonusurika. Awali iliripotiwa kuwa mrembo huyo alipata ajali kwasababu alikua akiendesha gari lake kwa kasi.
Chanzo kilichokuwa eneo la tukio kilisema kuwa Snura alikuwa kwenye mwendo wa kasi na kushindwa kukata kona iliyopo maeneo ya Cocacola Mikocheni.
Akizungumza na Risasi Mchanganyiko, Snura alipinga kuwa ajali aliyopata ilisababishwa na yeye kuendesha gari lake kwa kasi.
Snura alieleza kuwa alipoteza mwelekeo kwani hakua anajua hio barabara vizuri, alisema ajali hio ilitokea kwasababu hakujua kuna kona kali mbele.
“Unajua ajali ilikuwa mbaya sana, nashukuru waliotuokoa, chanzo cha ajali ni kwamba ile barabara siijui vizuri kwa hiyo sikujua pale kama kuna kona kali ndiyo maana nikapoteza mwelekeo. Kupona au kutoka hivi salama kwenye ile ajali ni Mungu tu, maana gari liliacha njia na kupinduka, lakini mimi na mdogo wangu tulipata michubuko midogo tu mwilini na sasa hivi tunaendelea vizuri tu,” alisema Snura.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.