Abraham Ntambara
KAMPUNI ya StarTimes imesema itaonyesha michuano ya Kombe la Mabara
yanayotarajia kuanza Juni 17 hadi Julai 2 mwa ka huu nchini Urusi.
Taarifa
iliyotolewa jana kwa vyombo vya habari na Ofisa Uhusiano wa Kampuni hiyo
Josephine Stephen, alisema mashindano hayo yatatumika kama maandalizi ya
mashindano ya kombe la dunia yatakayofanyika mwakani.
Kwa mujibu
wa taarifa hiyo ilisema mashindano haya yatakuwa ya kiwango cha juu ambapo mabingwa
wa kombe la dunia Ujerumani wanatarajia kupeleka timu yenye wachezaji vijana,
hivyo nchi nyingine zinaona kama ni fursa ya pekee.
Aidha ilisema kuwa nchi ya Ureno
ambayo ni mabingwa wa kombe la Ulaya watakuwa ikiongozwa na mchezaji wao nyota
Christian Ronaldo ambapo inataka kuweka historia katika mashindano hayo.
Lakini pia katika michano hiyo Arturo
Vidal na timu yake ya Chile ambao pia ni washiriki katika fainali hizo
hawatatamani kuondoka watupu.
Taarifa ilifafanua kundi B, litakuwa na timu ya Chile ambayo ndiyo inapewa nafasi
kubwa ya kuongoaza kundi hilo, lakini vijana wa Ujerumani watataka kuwaonyesha
kaka zao kuwa wako tayari kuchukua nafasi zao katika timu ya Taifa huku timu ya
Cameroon mabingwa wa Bara la Afrika wakiwa na matarajio madogo pamoja na timu
ya Australia.
Kundi A, litakuwa na timu za New Zealand,
Ureno, Mexco na mwenyeji Ureno ambayo itanufaika na uwepo wa mashabiki wake.
“Swali la uhakika ni kwamba: Je
mshindi atavunja mwiko wa wa kombe hili la Mabara? Tangu kuanzishwa mashindano
haya hakuna bingwa wa kombe hili aliyewahi kuwa mshindi wa kombe la dunia.
Mfano Brazil alishinda kombe hili mara tatu lakini hakufanikiwa katika
mashindano ya kombe la dunia yaliyofuata,” alisema Ofisa Uhusiano na Meneja
Masoko wa StarTimes Tanzania Juma Suluhu.
StarTimes kama mshirika rasmi wa
Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA) itaonyesha mashindano hayo kupitia
chaneli zake zote za michezo pamoja na channeli za ICC na DFL Supercup.
Aidha licha ya kuonyesha michuano
hiyo itatoa ofa maalumu katika kipindi cha msimu wa sabasaba za tamthilia
pamoja na program za watoto.
mwisho
Comments