Abraham Ntambara
VIONGOZI wa Dini wameombwa kusimama
mstari wa mbele katika kuhakikisha wanaisaidia serikali kwa kuhamasisha ili
kuendelea kufichua na kuwabaini wahalifu wanaendelea kujihusisha na mauaji ya
Kibiti, Mkoani Pwani na maeneo mengine.
Kauli hiyo ilitolewa jana jijini Dar
es Salaam na Mchungaji wa Mitume, Manabii na Maaskofu Tanzania Komando Mashimo
wa Huduma ya Njili ya Maumivu na Uponyaji wakati akizungumza na vyombo vya
habari, alisema suala hilo la mauaji halivumiliki.
Aidha alibainisha kuwa lengo la
kuomba viongozi wa dini kufanya hivyo
nikutokana na wao ndiyo waliobeba watu wengi katika Makanisa na Misikiti ambao ni
rahisi kwao kuwahamasisha na kuweza kutoa ushirikiano.
Alieleza kuwa kila kukicha watu wasio
na hatia wamekuwa wakiuawa huku viongozi wa hao wakishindwa kutilia mkazo
katika kulitafutia ufumbuzi wa suala hilo kwa kuisaidia serikali.
“Naomba viongozi wa dini wasimame kwa
pamoja wahamasishe makanisani mwao, tuilinde amani na kila mtanzania awe mlinzi
juu ya mwenzake, akimuona mwenzake anafanya mambo yasiyo faa, basi atoe taarifa
kwenye vyombo husika ili hatua ichukuliwe,” alisema Mashimo.
Aidha alisema Tanzania ina Manabii
988 ambapo alitoa rai kwa manabii hao kusimama na kueleza walipojificha
waharifu hao kwani wao husimama kama siko la Taifa.
Alifafanua kuwa kazi ya nabii ni
kutoa maelekezo ambapo alisema kuwa waache kutoa tu maji ya upako na badala
yake wajikite pia katika kulisaidia Taifa katika kutatua tatizo hilo la mauaji.
“Manabii watuambie watu hawa wako
wapi, wamejificha sehemu gani , kama kweli Mungu anawatumia watuambie kwani
kazi yao ni kuilinda nchi na kufichua yaliyofichika,” alisema.
mwisho
Comments