Wazungu Waliomuingiza Kijana Mweusi Kwenye Jeneza Wafikishwa Kortini


AFRIKA KUSINI: Wakulima wawili wazungu watafikishwa mahakamani nchini Afrika Kusini, baada ya kutuhumiwa kuwa walimsukuma kijana mmoja mweusi na kumuingiza ndani ya jeneza akiwa hai, huku wakitishia kumwagia mafuta ya petroli ili wamteketeze kwa moto.

Wakati Victor Mlotshwa alipokataa, wakulima hao walimtishia kuwa watamweka ndani ya jeneza hilo pamoja na nyoka.
Mlotshwa

Washtakiwa hao Willem Oosthuizen na Theo Jackson, walikamatwa mwezi Novemba 2016, baada ya video ya kitendo hicho kilipowekwa na kusambaa mitandaoni.
Walisema kuwa, Bwana Mlotshwa alipitia kwenye shamba lao liliko katika Jimbo la Mpumalanga, bila ya kuwa na idhini, na walikuwa wakimuadhibu.
Katika kusikizwa kwa kesi hiyo awali, jaji wa mahakama alisema kuwa wakulima hao walikuwa wakatili na waliojaa tabia za ubaguzi wa rangi.
Chanzo: BBC

TAZAMA VIDEO YA TUKIO HILO

Tupia Comment Yako, Matusi Hapana

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.