YANGA YAIPA ‘ZA CHEMBE’ SIMBA, YAMSAINI BUSWITA MIAKA MIWILI


Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
YANGA SC imeonyesha haiwezi kuzidiwa ujanja na mahasimu Simba kwa mchezaji yeyote wamtakaye, baada ya leo kufanikiwa kumsaini kiungo Pius Buswita kutoka Mbao FC ya Mwanza.
Juzi, Simba walitamba kumalizana na kiungo huyo anayeweza kucheza kama winga na mshambuliaji pia wakati tayari tetesi zilikuwa zimezagaa kwamba yuko kwenye rada za Yanga. 
Lakini baada ya ukimya wa saa 24, Yanga wanaibuka na jibu la kuwafunga kabisa mdomo mahasimu wao, Simba wakiwa wameingia mkataba na miaka miwili na mchezaji huyo aliyeng’ara katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu uliopita.
Pius Buswita (kushoto) akitia dole gumba kwenye fomu za Yanga. katikati ni Mhasibu wa klabu, Baraka Deusdedit 
Pius Buswita akitamba na mpira katikati ya wachezaji wa Simba katika mechi ya Ligi Kuu Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam

Rasmi huyo anatakuwa mchezaji wa pili kusajili Yanga baada ya beki wa Taifa ya Jang’ombe, Abdallah Hajji Shaibu, lakini habari zisizo rasmi zinasema hata kipa Mcameroon, Youthe Rostand naye amesaini ingawa haujapatikana uthibitisho wowote hadi sasa.
Wengine wanaotajwa kuwa kwenye mpango wa kusailiwa Yanga ni Babu Ally Seif kutoka Kagera Sugar, Ibrahim Hajib kutoka Simba na Himid Mao kutoka Azam FC.  

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA