Dege la kivita lililokuwa likifanya mazoezi katika anga la Dar es Salaam limesababisha mtafaruku mkubwa kwa wakazi jiji hilo.
Kitendo hicho kilitokea majira ya saa 3 asubuhi na kusababisha kila mmoja kuelezea kivyake kuhusu dege hilo lililokuwa na muungurumo mkubwa huku likiwa kwenye mwendo kasi na kimo cha chini.
"Mimi nilivyosikia muungurumo huo nilistuka na kuachia usukani na gari kupoteza mwelekeo kuelekea kwenye mtaro kabla ya kulizuia tena," alisema dereva huyo ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja.
Mteja mmoja aliyekuwa katika jengo kubwa la kibiashara la Quality Centre, Barabara ya Nyerere, alisema kuwa walikumbwa na hofu kiasi cha kufikiri kuwa dege hilo limetua ghafla kwenye jengo hilo, hali iliyosababisha watu wengi waliokuwemo huo kupatwa na viwewe wasijue la kufanya.
Baadhi walisikika kuwa huenda wanajeshi walikuwa wanaendelea na mazoezi ya kivita hasa ikizingatiwa kwamba jana Julai 25,ilikuwa Siku ya Mashujaa ambayo hata hivyo haikusherehekewa kama ilivyo kawaida miaka mingi iliyopita.
Rais John Magufuli ambaye ni Amiri Jeshi Mkuu akiwa mkoani Singida kwa ziara ya kikazi jana, aliwaomba wananchi kwenye mkutano wa hadhara kusimama kwa muda wa dakika moja kuwaombea dua wanajeshi wote walikufa vitani na kueleza kuwa mwaka huu Siku ya Mashujaa haitakuwepo bali itasherehekewa kwa wahusika kushiriki kwenye shughuli za kijamii.
Sababu za Siku hiyo ya mashujaa kutoadhimishwa mwaka huu hazikuweza kutajwa.
Kitendo hicho kilitokea majira ya saa 3 asubuhi na kusababisha kila mmoja kuelezea kivyake kuhusu dege hilo lililokuwa na muungurumo mkubwa huku likiwa kwenye mwendo kasi na kimo cha chini.
"Mimi nilivyosikia muungurumo huo nilistuka na kuachia usukani na gari kupoteza mwelekeo kuelekea kwenye mtaro kabla ya kulizuia tena," alisema dereva huyo ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja.
Mteja mmoja aliyekuwa katika jengo kubwa la kibiashara la Quality Centre, Barabara ya Nyerere, alisema kuwa walikumbwa na hofu kiasi cha kufikiri kuwa dege hilo limetua ghafla kwenye jengo hilo, hali iliyosababisha watu wengi waliokuwemo huo kupatwa na viwewe wasijue la kufanya.
Baadhi walisikika kuwa huenda wanajeshi walikuwa wanaendelea na mazoezi ya kivita hasa ikizingatiwa kwamba jana Julai 25,ilikuwa Siku ya Mashujaa ambayo hata hivyo haikusherehekewa kama ilivyo kawaida miaka mingi iliyopita.
Rais John Magufuli ambaye ni Amiri Jeshi Mkuu akiwa mkoani Singida kwa ziara ya kikazi jana, aliwaomba wananchi kwenye mkutano wa hadhara kusimama kwa muda wa dakika moja kuwaombea dua wanajeshi wote walikufa vitani na kueleza kuwa mwaka huu Siku ya Mashujaa haitakuwepo bali itasherehekewa kwa wahusika kushiriki kwenye shughuli za kijamii.
Sababu za Siku hiyo ya mashujaa kutoadhimishwa mwaka huu hazikuweza kutajwa.
Comments