HAJI MANARA AFUTIWA ADHABU YA TFF


Haji Manara.

KAMATI ya Nidhamu ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), chini ya mwenyekiti wake, Tarimba Abass, leo Jumatatu imefikia uamuzi wa kumfutia adhabu Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Simba, Haji Manara.
Kamati hiyo imefikia uamuzi huo baada ya Manara kuomba kupitiwa upya adhabu aliyopewa hapo awali ya kufungiwa kutojihusisha na soka kwa kipindi cha miezi 12 na kulipa faini ya Sh milioni 9.

Kutokana na kufutwa kwa adhabu hiyo, Manara kuanzia leo atakuwa huru kuendelea kufanya majukumu yake ya soka ndani ya Simba.
Mbali na Manara, kamati hiyo pia imewafutia adhabu Kaimu Katibu Mkuu wa Chama cha Soka Rukwa, Blassy Kiondo, Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi Rukwa, James Makwinya na Mwenyekiti wa Chama cha Soka Rukwa, Ayubu Nyaulingo,  ambao walikuwa wamefungiwa kutokana na kufanya uchaguzi wakati TFF iliwazuia.

Katika hatua nyingine, Tarimba amesema kuhusiana na adhabu ya Damas Ndumbaro, imeshindwa kupitiwa kutokana na kutopokea ombi la kuipitia, huku pia akiiomba TFF kuangalia kama kuna barua za watu mbalimbali walioomba kupitiwa kwa adhabu zao wazifikishe kwenye kamati yake ili waweze kuzifanyia kazi.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.