JAFO AKEMEA TATIZO LA MIMBA KWA WANAFUNZI WILAYA YA UKEREWE.


Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa Shule ya sekondari wasichana ya Bukongo wilayani Ukerewe.

Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa shule ya sekondari ya wavulana ya kidato cha tano na sita   ya Pius Msekwa wilayani Ukerewe.

Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo akizungumza na watumishi wa Halmashuari ya wilaya ya Ukerewe wakati akihitimisha ziara yake wilayani humo.

Watumishi wa halmashauri ya Ukerewe wakimsikiliza Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo. 
.................................................................................

Naibu Waziri wa nchi Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo amekemea tatizo la wanafunzi wa sekondari kupata mimba wakiwa shuleni ambapo hadi sasa kuna wanafunzi 108 ambao wamebainika kuwa na ujauzito kwenye wilayani Ukerewe.

Kauli hiyo ameitoa katika ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo kwenye sekta mbalimbali wilayani humo.

Jafo amewataka viongozi wote wilayani humo kuungana kupambana na tatizo hilo bila ya kuoneana aibu. 

Naibu Waziri huyo amewataka wanafunzi kuzingatia masomo kwani elimu ndio msingi wa maisha kwa mwanadamu yeyote.

Amewakemea wanafunzi wakike wenye tabia ya kujihusisha kwenye mapenzi wakiwa na umri mdogo na kwamba jambo hilo linahatarisha mustakabali wa maisha.

Katika ziara hiyo,Jafo alifanya ukaguzi wa ujenzi wa mabweni, madarasa, maabara, na vyoo kwa shule ya sekondari Pius Msekwa na sekondari ya Bukongo ambapo serikali ilipelekwa fedha mwezi April mwaka huu zaidi ya sh. milioni 500 ili kuwezesha elimu ya kidato cha tano na sita wilayani humo. 


Naibu Waziri Jafo amemaliza ziara yake wilayani Ukerewe mkoani Mwanza na kuelekea wilaya na Tarime na Rorya mkoani Mara.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI

KOCHA WA AL.AHLY ASEMA YANGA NI TIMU BORA NA NGUMU