Mwimbaji mkongwe nchini wa muziki wa dansi, Shaban Dede aliyefariki dunia jana asubuhi katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili alikokuwa amelazwa kwa siku kadhaa akitibiwa amezikwa leo katika Makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam.
Watu wamejaa nyumbani kwa Marehemu, Mtaa wa Congo/Kibambawe, Jaqngwani Karikaoo kwa ajili ya shughuli nzima ya kuaga na kuuzika mwili wa marehemu Dede.
Dede atakumbukwa kwa umahiri wa tungo zake za nyimbo kama vile Kilio Cha Mtu Mzima, Kaza Moyo (Msondo), Diana, Tui la Nazi, Amina (Sikinde), ambazo zinaonesha uhalisia wa maisha ya watu na zilijizolea umaarufu katika kumbi mbali mbali za muziki na kuvuta mashabiki wa rika zote.
Dede, alikuwa mwanamuziki mkubwa ambaye alikuwa akiitumikia Msondo Music Band lakini huko nyuma aling’ara na Bendi za Mlimani Park “Sikinde”, Bima Lee, alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya sukari pamoja na figo.
Na Richard Bukos | Global Publishers
Comments