AZAM ‘WALIAMSHA DUDE’ KAMPALA...MGHANA APIGA ZOTE MBILI URA WAFA 2-0 KWAO


Na Mwandishi Wetu, KAMPALA
TIMU ya Aza FC imepata ushindi wa kwanza katika ziara yake Uganda kujiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, baada ya kuwachapa wenyeji, URA mabao 2-0 katika mchezo wa kirafiki uliofanyika Uwanja wa Phillip Omondi, Kampaa jioni jioni ya leo.
Kocha Mkuu wa Azam FC, Aristica Cioaba, alichezesha kikosi kingine cha pili katika mchezo huo na kuwapumzisha wachezaji walioanza kwenye mechi mbili zilizopita wakitoa sare zote 2-2 na Uganda Kombaini na 1-1 na KCCA.
Mabao yote mawili ya Azam FC yamefungwa na mshambuliaji Yahaya Mohammed, moja katika kila kipindi cha mchezo huo, la kwanza akifunga dakika ya 19 kwa shuti kali nje ya eneo la 18 kabla ya kutupia jingine la aina hiyo dakika ya 47.
Yahya Mohammed (aliyepiga magoti) akipongezwa na Joseph Mahundi baada ya kufunga leo

Licha ya mabadiliko makubwa kikosini kwenye mchezo huo, bado timu hiyo ilionekana kucheza na kuwa imara kwenye eneo la ulinzi huku kipa Mwadini Ally, akifanya kazi kubwa baada ya kuokoa michomo mingi ya URA.
Mara baada ya mchezo huo wa tatu wa kirafiki kwenye kambi ya timu hiyo nchini Uganda ambapo jana ikitoka sare ya bao 1-1 na mabingwa wa Uganda KCCA, Azam FC itashuka tena dimbani Jumapili ijayo kumenyana na Onduparaka, mtanange utakaofanyika Uwanja wa Nambole kuanzia saa 10.00 jioni.
Ziara hiyo itahitimishwa Jumatatu ijayo kwa Azam FC kucheza mchezo wa tano wa kirafiki dhidi ya washindi wa tatu wa Ligi Kuu Uganda msimu uliopita, Vipers FC, utakaofanyika Uwanja wa St Marys uliopo Kitende, Uganda.
Kikosi cha Azam FC leo kilikuwa: Mwadini Ally, Swaleh Abdallah, Hamimu Karim, Abdallah Kheri, David Mwantika, Stephan Kingue, Idd Kipagwile/Braison Raphael dk57, Salmin Hoza/Frank Domayo dk84, Yahaya Mohammed/Yahya Zayd dk70, Enock Atta Agyei/Masoud Abdallah dk55 na Joseph Mahundi/Ramadhan Singano dk81.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI