Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Pombe Magufuli, amemaliza bifu kubwa lililokuwepo kati ya Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media, Ruge Mutahaba na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kwa kuwakutanisha wawili hao jukwaani na kuwataka washikane mikono.
Tukio hilo la aina yake, limetokea leo AGOSTI 5, 2017 kwenye Kijiji cha Chongoleani, Tanga ambapo kulikuwa na tukio kubwa la uwekaji wa jiwe la msingi kwenye mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta kutoka Hoima, Uganda mpaka kwenye Bandari ya Tanga.
Tazama Ruge na Makonda Wakicheza Muziki Baada ya Kupatanishwa na Rais Magufuli
Rais Magufuli Alivyomaliza Bifu la Makonda na Ruge
Akawataka wawili hao, kwa kuwa wote ni vijana, wamalize tofauti zao na kuchapa kazi kwa bidii kwani anawapenda wote wawili, kitendo kilichoibua shangwe kubwa kwa watu waliokuwepo kwenye tukio hilo.
Chanzo cha ugomvi wa wawili hao, yalikuwa ni madai ya Makonda kuvamia kwenye ofisi za Clouds FM akiwa na askari wenye silaha, akidaiwa kushinikiza kipindi alichokuwa na maslahi nacho kirushwe hewani, jambo lililosababisha vuguvugu kubwa miongoni mwa waandishi wa habari na wananchi kwa jumla.
Comments