SIRI ZA CHUMBANI ZA KIDOA ZAANIKWA


SIRI ZA CHUMBANI ZA KIDOA
Kidoa
MSANII wa filamu ambaye ndiye The Ijumaa Sexiest Girl 2015, Asha Salum ‘Kidoa’ amegandwa na madai ya kuwa bonge nyanya tofauti na alivyokuwa huko nyuma kiasi cha kuathiri uwezo wake awapo faragha.

Akipiga stori na Risasi Vibes mmoja wa mashosti wa staa huyo aliyeomba hifadhi ya jina lake alidai kuwa, mara kwa mara Kidoa amekuwa akijilaumu kwa kushindwa kuukontroo mwili wake huku akihofia kuachwa na ‘baby’ wake.

“Unajua sasa hivi Kidoa amekuwa bonge sana na anahisi hata mpenzi wake atamuacha maana yale mambo ya chumbani atakuwa hayamudu,” alimwaga siri za chumbani za kidoa  sosi huyo. Katika kujua ukweli wa ishu hiyo, paparazi wetu alimtafuta Kidoa na alipobanwa juu ya madai hayo alifunguka:

“Mh! Aliyewaambia hayo ni mmbeya sana, hata niwe bonge vipi bado siwezi kushindwa kujimudu faragha. Mimi ni msichana niliyefundwa, ni mtundu na mbunifu, hata mpenzi wangu anajua hilo. Kuhusu ubonge, nafanya jitihada za kurudisha ule mwili wangu na umbo namba nane,” alisema Kidoa.

NA: MAYASA MARIWATA

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*