TANZIA;MPIGANAJI ATHUMAN HAMISI AMEAGA DUNIA!!!

TANZIA 
Ndugu yetu, Rafiki yetu na Mpigapicha Athumani Hamisi Msengi amefariki dunia Alfajiri ya leo baada ya kuugua ghafla akiwa Nyumbani kwake Sinza na kukimbizwa Hospitali ya Taifa Muhiumbili alipofikwa na umauti asubuhi ya leo.

Marehemu amewahi kufanyakazi vyombo mbalimbali vikiwemo The Guardian, Nipashe na Habari Leo;ambapo kwenye Habari alikuwa Mpiga Picha Mkuu wakati lilipoanzishwa mwaka 2006.

Aidha kwenye kampeni za Urais za JK mwaka 2005 marehemu alikuwa ndiye Mpigapicha rasmi wa mgombea huyo.


Akiwa Habari Leo alipata ajali ya gari barabara ya Kilwa, mkoani Pwani alikoenda kwenye kazi za Vodacom,ajali ambayo ilimsababishia kupooza kuanzia kiunoni kushuka chini. Ugonjwa ambao ulimlaza kitandani tangu wakati huo mpaka kifo chake.

Amewahi kutibiwa hospitali mbalimbali zikiwemo na hapa nchini na Afrika Kusini kwa msaada wa Rais Mstaafu JK.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.