Daunguro 'kubwa zaidi' la makahaba barani Asia lapata sura mpya


Muonekano wa jumla wa mtaa wa makahaba wa SonangachiHaki miliki ya pichaEPA
Image captionPicha ya jengo lenye mchoro katika mtaa wa Sonangachi wa makahaba katika wilaya ya Kolkata
Wasanii wa michoro wasiokubali jinsia ya maumbile yao wamekuwa wakiipatia sura mpya ya michoro ya rangi za kuvutia wilaya yenye idadi kubwa ya makahaba ya Sonagachi iliyopo katika jiji lililopo mashariki mwa India la Kolkata (zamani likiitwa Calcutta).
Picha hiyo juu inaonyesha mchoro uliochorwa kwenye jengo la chama cha ushirika cha makahaba.
Ikisemekana kuwa wilaya yenye idadi kubwa zaidi ya mahahaba bara Asia, Sonagachi ni wilaya yenye mitaa yenye barabara nyingi nyembamba na njia za uchochoroni kati kati mwa jiji la Kolkata, ikiwa ni makazi ya makahaba takriban 11,000.
Indian commuters walk past a painted building at Sonagachi red light district in Kolkata,Haki miliki ya pichaEPA
Wakifanya kazi kwa ushirikiano na wasanii wenye makao yao Bangalore, wasanii wa michoro wasiokubali maumbile yao ya jinsia (transgender) walichora michoro kwenye michoro ya rangi za kuvutia kwenye baadhi ya majengo kama sehemu ya kampeni ya kuhamasisha umma kuhusu haki za makahaba na pia kujaribu kuzuia unyanyasaji dhidi ya wanawake.

Uchoroji wa michoro hii ulichukua muda wa wiki nzima

Mengi kati ya madanguro haya yamechakaa.
Wapitanjia katika mtaa wa makahaba katika wilaya Sonagachi jijini KolkataHaki miliki ya pichaEPA
Image captionWapitanjia wa Kihindi wakipita kwenye mtaa wa madanguro ya makahaba yenye michoro katika wilaya ya Sonangachi jijini Kolkata
Kuta katika mtaa wenye majengo yaliyosongamana pia zilipakwa rangi.
Wapitanjia katika mtaa wa makahaba katika wilaya SonagachiHaki miliki ya pichaEPA
Hapa wapitanjia na wafanyabiashara wanaonekana kwenye moja ya jengo lililopigwa rangi.
Kuna mipango ya kuyapaka rangi majengo zaidi katika wilaya ya Sonangachi.
Indian commuters walk past a painted wall at Sonagachi red light district in KolkataHaki miliki ya pichaEPA
Ukahaba umesalia kuwa tatizo kubwa kwa India, ambako wanawake milioni tatu wanaaminiwa kufanya biashara ya ukahaba.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*