Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Hope For All (Washona Mahema), Askofu Edger Mwamfupe (kushoto) akiwachangamsha washiriki kabla ya kuanza kutoa mada kuhusu Ujasiri Kilimo wakati wa Mafunzo ya Usimamizi wa Shamba la Papai Salama yaliyoandaliwa na Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania (Mkikita) kwenye Ukumbi wa Anatoglou, Mnazi Mmoja, Dar es Salaam. Mkikita na Washona Mahema wameunda umoja wa Kilimo Viwanda Tanzania (KIVITA) utakaokuwa unatoa mafunzo ya kuwajengea uwezo wakulima nchini.
Mtaalamu wa Kilimo, John Charles akitoa mada kuhusu mfumo wa umwagiliaji kwenye kilimo cha papai salama wakati wa mafunzo hayo. Imeandaliwa na Richard Mwaikenda: Kamanda wa Matukio Blog;0715264202,0754264203,0689425467
Wanafunzi wa Chuo cha Kilimo na Malisili cha Canre, Dar es Salaam, Kogea Levi (kulia) na Frank Godson wakiwa makini kusikiliza mada kuhusu kilimo cha papai salama
Sehemu ya washiriki wa mafunzo hayo
Sehemu ya washiriki wa semina hiyo
Mkurugenzi wa Masoko na Utafiti wa Mkikita, Deo Liganga (kulia) akiwa na Mtaalamu wa Kilimo wa Mkikita, Samweli pamoja na Simeo aliyetoa mada kuhusu usimamizi wa kilimo cha Papai Salama.
Wafanyakazi wa Mkikita wakijadiliana jambo wakati wa mafunzo hayo. Kutoka Kushoto ni Meneja Uhusiano, Neema Ngowi, Mkurugenzi wa Fedha na Utawala, Elizabeth Ndamgoba na Mhasibu Msaidizi, Samson Kalinga.
Adam Ngamange akiwa na badhi ya wadau wakati wa mafunzo hayo
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Hope For All (Washona Mahema), Askofu Edger Mwamfupe (kushoto) akiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania (Mkikita), Adam Ngamange, alipokuwa akitoa mada kuhusu Ujasiri Kilimo wakati wa Mafunzo
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Hope For All (Washona Mahema), Askofu Edger Mwamfupe (kushoto) akiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania (Mkikita), Adam Ngamange, alipokuwa akitoa mada kuhusu Ujasiri Kilimo wakati wa Mafunzo ya Usimamizi wa Shamba la Papai Salama kwenye Ukumbi wa Anatoglou, Mnazi Mmoja, Dar es Salaam. Mkikita na Washona Mahema wameunda umoja wa Kilimo Viwanda Tanzania (KIVITA) utakaokuwa unatoa mafunzo ya kuwajengea uwezo wakulima nchini.
Mwenyekiti wa Kikosi Kazi cha Uundwaji wa Ushirika wa Tanzania Holtculture Iniciative Society (THIS), Abraham Nyantory akielezea muundo wa Rasimu ya Katiba hiyo kwa wanachama watarajiwa wa ushirika huo utakaokuwa chini ya mwamvuli wa Mkikita.
Comments