ZAKIA MEGHJI AWATIA HAMASA GIRL GUIDES, ATAKA WAWE JASIRI

 Mjumbe wa Bodi ya wadhamini ya Chama cha Tanzania Girl Guides (TGGA), Zakia Meghji akitoa maneno ya hamasa kwa vijana wa Girl Guides katika semina iliyofanyika Makao Makuu ya TGGA, Mtaa wa Kibasila, Upanga Dar es Salaam.

Meghji ambaye aliwaelezea historia ya maisha yake tokea utotoni, shuleni, chuoni na ya kisiasa, aliwataka Girl Guides kuwa jasiri, waadilifu, wazalendo na wachapakazi pamoja na kuwa na vision..

Aliwafundisha jinsi ya kupambana na wanaume walaghai wanaowataka kimapenzi na kuwaharibia ndoto yao ya kielimu na maisha kwa ujumla.

Pia aliwataka kuheshimu mila nzuri, desturi na utamaduni mzuri pamoja na kuwaheshimu wazazi na jamii bila kusahau kushirikiana nao katika masuala mbalimbali.

Aliwaambia kuwa baadhi ya mambo muhimu ni kuwa na tabia ya kushirikiana na watu mbalimbali kwa lengo la kubadilisha uzoefu, mawasiliano na kwamba unatakiwa kuanza uongozi ukiwa kijana siyo ukiwa mzee.

Anawaeleza kuwa ushupavu wake ulimfanya kwa mara ya kwanza awe mbunge mwaka 1985, amekuwa Mkuu wa wilaya na waziri kwa muda mrefu mpaka alipoamua kustaafu.

 IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG;0715264202,0754264203,0689425467
 Girl Guides wakiimba wimbo wa hamasa
 Kamishna wa Kimataifa wa TGGA, Miryam Mjema akisalimiana na Girl Guides kutoka shule mbalimbali za Dar es Salaam na mikoani.
 Mkufunzi wa TGGA Makao Makuu ya TGGA,  akielezea historia ya chama hicho
 Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini wa TGGA, Grace Makenya akitoa maneno ya hamasa kwamba daima hastaafu na kwamba yeye hivi sasa ana miaka 70 lakini bado ni Girl Guides

 Girl Guides wakiimba wimbo wa hamasa
 Yess Girl, Nadine Ratovoson kutoka Madagascar akijitambulisha. Yupo nchini kwa ziara ya mafunzo ya miezi sita ya kubadilishana mafunzo.
 Yss Girl kutoka Zambia ambaye yupo nchini kwa ziara yamiezi sita ya  kubadilisha mafunzo
 Miryam Mjema na Grace Makenya
 Kamishna wa TGGA, Temeke, Komba akijitambulisha
 Sophia Simon (kulia) Mkufunzi wa TGGA Temeke, akijitambulisha
 Kamishna wa TGGA Ilala, Stellah Kasisika akijitambulisha
 Girl Guide wakiwa na furaha
 Meghji akisisitiza jambo
 Kamishna Mkuu wa TGGA,  Symphorosa Hangi (kulia) akiwa na Mdau wa TGGA, Asiah Abdul Azizi na Candida Bahame.
Mwanafunzi kutoka Shule ya Zanaki, Winhope Mgalega, akimmuliza Zakhia Meghji ni nini siri ya mafanikio yake.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

ALLY KAMWE AZIMIA KWA MKAPA.

RAIS SAMIA KUZINDUA MKUTANO MKUU WA 79 WA BARAZA LA MICHEZO YA MAJESHI DUNIANI

MIGINGO KISIWA KIDOGO ZAIDI AFRIKA KILICHOGOMBEWA NA UGANDA, KENYA