Inaelezwa kuwa wazazi hao ambao wana watoto saba wa kike waliamua kumlazimisha mtoto wao huyo kuishi kama mvulana, kwa kumvalisha kiume na kumfanya afanye kazi za kiume kwa madai kwamba japo hawajapata mtoto wa kiume, mtoto wao huyo ndiye atakuwa wa kiume.
Binti huyo ambaye anajulikana kwa jina la Sitara Wafadar anaeleza kuwa baba yake anamchukulia kuwa yeye ndiye mtoto wake wa kiume mkubwa na hata wakati mwingine humtuma akamwakilishe misibani kama mvulana, jambo ambalo kwa jamii zao mshichana hawezi kufanya.
Sitara anafanya kazi na baba yake ya kufyatua matofali ili kuilisha familia yao kwa siku sita za wiki, kwa saa sita kwa siku.
Comments