Aliyekua Rais wa Afrika Kusini Comrade Jacob Zuma, Mapema leo amepandishwa kizimbani katika mahakama kuu Mjini Durban Kujibu tuhuma za Ufisadi na Rushwa Zinazomkabili, Ikumbukwe kuwa ni Februari 14 Mwaka huu amabapo Zuma alilazimika kujiuzulu kwa shinikizo la chama chake akituhumiwa kwa makosa mbalimbali ya Rushwa, ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka.
Baada ya kusomewa mashtaka 16 yanayomkabili Comrade Zuma yakiwemo Rushwa, udanganyifu na kujitajirisha kinyume cha sheria, Jaji wa mahakama hiyo kuu mjini Darban, Themba Sishi ameihairisha Kesi hiyo mpaka Juni 8, 2018 itakapotajwa tena.
#MyOpinion
Watawala karibu wote tu katika Afrika wanafanana kwa tabia za wizi wa mali za umma (Ufisadi) na matumizi mabaya ya madaraka, Kwahivyo si vyema sana kwa baadhi ya nchi za Afrika (Tanzania ikiwemo) kuendelea kuweka kinga kwa Maraisi wao kutokushtakiwa wakishaondoka madaraka.
Watawala karibu wote tu katika Afrika wanafanana kwa tabia za wizi wa mali za umma (Ufisadi) na matumizi mabaya ya madaraka, Kwahivyo si vyema sana kwa baadhi ya nchi za Afrika (Tanzania ikiwemo) kuendelea kuweka kinga kwa Maraisi wao kutokushtakiwa wakishaondoka madaraka.
Comments