MANCHESTER City jana waliishindwa tena Liverpool baada ya kuambulia kichapo cha mabao 2-1 na kuondolewa kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya
(Uefa), huku Barcelona akipigwa 3-0 na Roma.
Katika mchezo wa kwanza Man City walichapwa mabao 3-0 kwenye Dimba la Anfield wiki moja iliyopita na jana walitakiwa kushinda mabao 4-0, ili wafuzu kwa hatua ya nusu fainali lakini wakaishia kupata kipigo hicho.
Hii ina maana kuwa Liverpool sasa wamefanikiwa kufuzu kwa hatua ya nusu fainali kwa mara ya kwanza kwa miaka ya hivi karibuni wakiwa wamewafunga City jumla ya mabao 5-1.
City walianza kwa kushtukiza baada ya kufanikiwa kufunga bao lao pekee kwenye mchezo huo katika dakika ya pili tu, kupitia kwa Gabriel Jesus, baada ya mabeki wa Liverpool kufanya uzembe.
Hata hivyo, Liverpool walishindwa kuonyesha kiwango chao cha kawaida kipindi cha kwanza na kuwaacha City ambao walitawala mchezo huo na kukosa nafasi kadhaa za wazi.
Katika dakika ya 40, City walifunga bao lakini mwamuzi akalikataa kutokana na kipa wa Liverpool kufanyiwa
madhambi hali iliyomfanya kocha Pep Guardiola kuwafokea waamuzi wakati wa mapumziko na kuondolewa kwenye benchi ambapo kipindi cha pili alikuwa jukwaani.
Kipindi cha pili, City waliingia kama wachovu baada ya kuonyesha kiwango cha chini na katika dakika ya 56, Liverpool walisawazisha kupitia kwa Mohamed Salah baada ya kazi nzuri iliyofanywa na Saidio Mane.
Wakati City wakipambana kutafuta mabao mengine, Robeto Firmino alikuwa shujaa baada ya kuifungia timu yake bao la pili katika dakika ya 77 na kuifanya Liverpool kuwa imeshawachapa City mara tatu msimu huu, baada ya kuwa timu ya pili iliyoifunga kwenye ligi hadi sasa.
Katika mchezo mwingine wa ligi hiyo, Barcelona walishangaza dunia baada ya kuchapwa mabao 3-0 na Roma, na kutupwa nje kwa sare ya mabao 4-4, baada ya Barca kushinda 4-1 kwenye mchezo wa kwanza katika Dimba la Camp Nou.
Hii ni mara ya kwanza Barcelona wanapata kichapo kikubwa hivi msimu huu kwenye Ligi ya M a b i n g w a Ulaya na kin a k u w a k ama historia kwao.
Edin Dze ko alikuwa tena shujaa kwenye timu yake baada ya kuifungia bao la kwanza katika dakika ya sita tu ya mchezo. Dakika ya 57 staa wa Roma, De Rossi, aliifungia timu yake bao la pili kwa mkwaju wa penalti.
Wakati Barcelona wakipoteza muda, dakika ya 82 maajabu yalitokea kwenye soka baada ya Manolas kuifungia Roma bao la tatu kwa kichwa na kuwaamsha mashabiki jukwaani.
Hii ina maana kuwa Roma wamefuzu kwa hatua hiyo kutokana na faida ya bao la ugenini.
ROMA:
Alisson 7; Juan Jesus 7, Manolas 7, Fazio 5; Kolarov 5, Nainggolan 6 (El
Shaarawy 77, 7) , De Rossi 8, Strootman 7, Florenzi 7; Schick 7 (Under
72, 7), Dzeko 9
Subs not used: Pellegrini, Gonalons, Peres, Skorupski, Gerson
Goals: Dzeko 6, De Rossi (pen) 58, Manolas 82
Booked: Fazio, Jesus
BARCELONA:
Ter Stegen 7; Semedo 6 (Dembele 85), Pique 5, Umtiti 5, Alba 6;
Busquets 6 (Alcacer 85), Rakitic 6, Sergi Roberto 5, Iniesta 6 (Gomes
81); Messi 6, L Suarez 6
Subs not used: D Suarez, Cillessen, Paulinho, Vermaelen
Booked: Pique, Messi, L Suarez
Manchester City (3-1-4-2):
Ederson 6, Walker 6, Otamendi 5.5, Laporte 5, Bernardo 6.5 (Gundogan
74, 6), Fernandinho 7, De Bruyne 7, Silva 6 (Aguero 66, 6), Sterling 7,
Jesus 6.5, Sane 7
Subs not used: Bravo, Kompany, Delph, Zinchenko, Foden
Goalscorers: Jesus 2
Booked: Ederson, Bernardo
Manager: Pep Guardiola 4
Liverpool (4-3-3):
Karius 6.5, Alexander-Arnold 6.5 (Clyne 81), Lovren 7, van Dijk 6,
Robertson 7, Oxlade-Chamberlain 6, Wijnaldum 6, Milner 7, Salah 6.5
(Ings 89), Firmino 8 (Klavan 81), Mane 7
Subs not used: Mignolet, Moreno, Solanke, Woodburn
Goalscorers: Salah 56, Firmino 77
Booked: Mane, Alexander-Arnold, Firmino, van Dijk
Manager: Jurgen Klopp 7
Referee: Antonio Miguel Mateu Lahoz
Comments