Mvua kubwa Dar es Salaam yatatiza usafiri wa mabasi ya mwendokasi


Mabasi ya mwendo wa kasi TZ
Image captionMabasi ya mwendo wa kasi TZ

Mvua kubwa inayonyesha Dar es Salaam Tanzania hivi sasa imetatiza huduma za usafiri kwa mabasi ya mwendokasi.
Usafiri wa mabasi hayo umesitishwa kutokana na mafuriko eneo la Jangwani.
Muandishi wa BBC Mjini Dar es Salaam anaeleza kuwa kila mvua kubwa inaponyesha huduma za mabasi hayo husitishwa kutokana na sababu kadhaa.
Mojawapo ya sababu ni kufurika maji kwa njia ambazo mabasi hayo yanapitia na pia kufurika maji kwenye kituo hicho kikuu ambapo mara ya mwisho mabasi kadhaa yaliharibika sababu ya kujaa maji.
Sababu nyingine ni kukatika kwa umeme kwenye vituo vyake wakati wa mvua - hivyobasi kusababisha kukwama kwa mfumo wake wa ukataji tiketi.
Hii sio mara ya kwanza kwa mabasi hayo ya mwendo kasi yalioanza kuhudumu Tanzania mnamo Mei mwaka 2016 mjini Dar es Salaam, kukabiliwa na athari za mvua kubwa.
Mwaka jana mkuu wa kitengo cha mawasiliano cha kampuni ya usafiri wa mabasi hayo - Udart, Deus Bugaywa alieleza kuathirika kwa mabasi 29 kati ya 134 baada ya maji kuingia katika sehemu tofuati za magari hayo zikiwemo injini.
Kwa sasa taarifa kutoka baadhi ya vyombo vya habari nchini zinasema huduma ya usafiri wa mabasi hayo imesitishwa kutoka na kwenda katikati ya jiji la Dar es Salaam na kwamba itarudishwa pindi hali itakapoimarika.

Mada zinazohusiana

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI