Raia wa Afrika Kusini watoa heshima za mwisho kwa marehemu Winnie Mandela


Raia wa Afrika Kusini wamuaga Winnie Mandela
Image captionRaia wa Afrika Kusini wamuaga Winnie Mandela
Maelfu ya watu wamekusanyika nchini Afrika Kusini kwa mazishi ya mwanaharakati wa kampeni dhidi ya ubaguzi wa rangi nchini humo Winnie Madikizela-Mandela.
Maelfu ya waombolezaji walikusanyika katika uwanja wa michezo wa Soweto karibu na mji mkuu wa Johannesburg ambapo Winnie Mandela anazikwa.
Jeneza lake lilifunikwa na bendera ya taifa hilo na rais wa Afrika Kusini alisoma kumbukumbu ya marehemu.
Bi Madikizela Mandela , ambaye ni mke wa zamani wa Nelson Mandela alifariki mapema mwezi huu akiwa na umri wa miaka 81.
Maria Nyerere anavyomkumbuka Winnie Mandela
Bi Madikizila Mandela alipongezwa kwa mchango wake wakati wa kukabiliana na ubaguzi wa rangi nchini Afriika Kusini.
Lakini baadaye aliipuuzwa na wanasiasa wakuu kwa kuunga mkono mauaji ya majasusi wa serikali.
Winnie Mandela alikuwa nani hasa?
Mwana wa Madikizela Mandela , Zenani Mandela Dlamini aliwashutumu wale aliotaja walikuwa na kampeni mbaya ya kumchafulia jina mamake na kumtenga kabla ya kumsafishia jina baada ya kifo chake.
''Inakera kuona vile walivyomchukulia wakati wa maisha yake, wakijua vile walivyomuumiza. Wanajua ni kwa nini waliamua kuanza kusema ukweli baada ya kifo chake'', alisema Bi Mandela Dlamini.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI