Rais Magufuli asisitiza umuhimu wa kuendelea kuwepo Muungano wa nchi


Rais wa Tanzania,Dokta John MagufuliHaki miliki ya pichaIKULU
Image captionRais wa Tanzania,Dokta John Magufuli
Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli amesisitiza haja ya watanzania kuendelea kudumisha amani na wasikubali kutumika kuivuruga amani ya nchi.
Katika maadhimisho makuu huko mjini Dodoma ya miaka 54 tangu Tanganyika na Zanzibar zilipoungana na kuunda Tanzania, Rais Magufuli amesisitiza umuhimu wa kuendelea kuwepo kwa Muungano wa nchi.
Licha ya kwamba kumekuwa na mazungumzo kuhusu maandamano dhidi ya Rais wa Tanzania Dokta John Magufuli ambayo yaliopangwa kufanyika leo, hali imekuwa shwari.
Kumekuwa na utulivu wa kawaida katika baadhi ya maeneo nchini licha ya kwamba kumekuwa na mazungumzo kuhusu maandamano dhidi ya kiongozi huyo na utawala wake.
Ndani ya mkoa wa kibiashara wa Dar es Salaam, wakaazi wamekuwa wakiendelea na shughuli mbalimbali kama kawaida.
Image captionKumekuwa na ukimya katikati mwa mji wa Dar es Salaam wakati siku za kawaida watu hupishana
Ulinzi mkali umeimarishwa sehemu mbalimbali nchini kwa ajili ya kuwa tayari kukabiliana na jambo lolote litakalo onekana kuhatarisha amani.
Kwa zaidi ya mwezi mmoja sasa, mwanaharakati wa kwenye mitandao ya kijamii, mtanzania ambaye makaazi yake ni nchini Marekani amekuwa akiratibu maandamano kupitia ukurasa wake wa Instagram.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*