Uganda yaomboleza kifo cha Sokwe mkubwa zaidi nchini


Mbali na kuhifadhiwa, Sokwe huwa bado wanakuwa hatariniHaki miliki ya pichaTERENCE FUH NEBA, WWF CENTRAL AFRICAN REPUBLIC
Image captionMbali na kuhifadhiwa, Sokwe huwa bado wanakuwa hatarini
Ijumaa kutakuwa na mkesha kuomboelza kifo cha Sokwe mkubwa zaidi nchini Uganda ambaye amekufa akiwa na miaka 54
Mwaka 1964, zakayo alikuwa na mwaka mmoja alipokutwa ametelekezwa magharibi mwa Uganda.Kituo cha elimu ya Hifadhi ya wanyamapori kimesema kuwa alitunzwa na wataalam na baadae alifikishwa kwenye hifadhi ya taifa akiwa na miaka 13.
Zakayo aliishi sehemu kubwa ya maisha yake katika hifadhi ya Entebbe, ingawa hapo kwa mujibu wa mamlaka nchini humo, alikuwa hatarini.Watalii walikuwa wanampa sigara na pombe ili awafurahishe.
Hifadhi hiyo kwa sasa imeboreshwa na Zakayo anayeitwa 'Babu' wa Sokwe wote nchini Uganda aliweza kuishi kwa raha
Wataalam wa uhifadhi wamemsifu Zakayo kwa kuwa balozi wa sokwe na wanyama wengine nchini Uganda.Wanasema wasifu wake ulisaidia kujipatia fedha kwa juhudi za uhifadhi na kuongeza idadi ya watalii
Mabaki ya Zakayo yatatunzwa kwa ajili ya utafiti na elimu.
Sokwe barani Afrika
Maisha ya Sokwe katika misitu barani Afrika hutegemea miti.
wanasayansi wameeleza hayo kutokana na utafiti walioufanya
utafiti ulibaini kuwepo kwa sokwe wengi kuliko wanyama wengine.
Sokwe katika nchi ya Cameroon,Afrika ya kati na Congo wanakabiliwa na tishio la ujangiliHaki miliki ya pichaEMMA STOKES/WCS
Image captionSokwe katika nchi ya Cameroon,Afrika ya kati na Congo wanakabiliwa na tishio la ujangili
Hata hivyo , wanyama hao wengi wako kwenye maeneo yasiyo na usalama,ambapo huwa hatarini kuuawa na majangili,Ebola na uharibifu wa mazingira
Hali hiyo pia imewakuta sokwe wa kwenye misitu ya nchini Cameroon,Afrika ya kati ,Jamuhuri ya kidemokrasia ya Congo, Guinea ya Ikweta na Gabon.
Silaha inamaanisha uwindaji: vijidudu inaamisha Ebola:na miti inaashiria kuwa wanyama wanahitaji msitu kuweza kuishi,amesema Dokta Fiona Maisels,Mwanasayansi wa hifadhi kutoka taasisi ya hifadhi ya wanyama.
Ikiwa misitu itakatwa.Ikiwa misitu itabadilishwa na kuwa kwa ajili ya kilimo, hakutakuwa na sokwe.
Kwa mujibu wa jarida la kisayansi, Watafiti wa kimataifa wanasema viumbe wa aina hii wanahitaji uangalizi zaidi ya wanaoupata.
Jitihada za uhifadhi lazima zizingatie kuimarisha hatua za kupiga vita ujangili, hatua za kudhibiti magonjwa na kutunza mazingira, wameeleza.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA