Vurugu za kudai maslahi zaibuka Afrika Kusini


South Africa
Image captionRaisi wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa
Rais wa Afrika Kusini , Cyril Ramaphosa, amekatisha ziara yake alipokuwa kwenye mkutano wa jumuiya ya madola nchini Uingereza ili kukabiliana na maandamano na vurugu nchini mwake.
Rais Ramaphosa aliitumia ziara yake kujaribu kuwashawishi baadhi ya wajumbe wa mkutano huo kuwekeza nchini mwake, ziara hii ni ya kwanza kimataifa baada ya kutwaa madaraka kutoka kwa raisi mstaafu Jacob Zuma mnamo mwezi Februari mwaka huu.
Lakini mapigano yameongezeka zaidi ya siku mbili katika jimbo la Kaskazini Magharibi.waandamanaji wanadai fursa ya ajira na makaazi na pia wanataka kuona rushwa inakomeshwa nchini mwao.
Barabara zimefungwa, magari yanachomwa moto na maduka yanavunjwa hovyo na wakaazi wa eneo hilo wametoa wito wa kujiuzulu kwa waziri mkuu wa jimbo.
Rais Ramaphosa amewataka waandamanaji kutulia na kuwataka polisi kuanza zoezi la kuzuia maandamano mapya.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.