Akizungumza katika Tamasha la Single Mothers lililoandaliwa na msanii mwenzake, Faiza Ally na kufanyika katika Hoteli ya De Mag iliyopo Mwananyamala, Dar, Wastara alisema kuwa, siri kubwa ya ndoa zake kuvunjika ni kutokana na kukosekana kwa maelewano ndani ya nyumba na siyo kwamba huwa anapenda kuachika.
“Unajua kuna vitu ambavyo ningevikubali kuvifanya nilipokuwa ndani ya ndoa, ungekuta sasa hivi nimeshakufa hivyo kuolewa na kuachika siyo kupenda, bali nilishindwa kukubaliana na mambo ambayo nilikuwa ninalazimishwa kuyafanya,” alisema Wastara wakati akizungumza na wamama hao ambao wanawalea watoto bila baba zao.
Hata hivyo, aliwataka wamama hao kuwa na ujasiri wa kufanya kazi kwa bidii na wasinyong’onyee kwa sababu ya kuwa wanawalea watoto peke yao baada ya kuzalishwa na wanaume kuwakimbia au kuachika katika ndoa.
STORI:GLADNESS, Mallya
Comments