Wananchi wa Mkoa wa Dar es salaam wameendelea *kula Matunda* ya serikali ya awamu ya tano baada ya *Rais Dr. John Magufuli* kutoa zaidi *Shilingi Billion 250* kwaajili ya utekelezaji wa *Miradi Mkakati* ya *kuziwezesha Halmashauri* za jiji hilo *kujiendesha zenyewe* ili kupunguza *utegemezi* wa fedha kutoka Serikali kuu.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam *Mhe. Paul Makonda* amesema miongoni mwa *miradi* itakayotekelezwa ni pamoja na *ujenzi wa kituo cha kisasa cha Mabasi ya Mikoani Mbezi Luis* kitakachogharimu zaidi ya shilingi *Billion 50* ambacho ujenzi wake utaanza *Mwezi June* na kuchukuwa *miezi 18* kukamilika.
*RC Makonda* amesema jengo hilo litakuwa na *gorofa tano* ambapo kituo hicho cha kisasa kitakuwa na uwezo wa kuchukuwa *Mabasi 200* na Maegesho *magari 300* (Underground parking) ambapo ndani kituo kutakuwa na huduma zote muhimu ikiwemo *Hotel, Hostel, Shopping Mall,Maduka, Migahawa, sehemu za mapumziko, Kituo cha Polisi, Bustani, Bank, Vyoo* vya kisasa pamoja na *Ofisi za kampuni za Magari.*
Aidha *RC Makonda* amesema miradi mingine ni Ujenzi wa *Soko la kisasa Kisutu* litakalogharimu shilingi *Billion 16*, Kituo cha Mabasi *Chamanzi Mkondogwa*, Ujenzi wa *Machinjio ya kisasa Vingunguti* yenye thamani ya *Billion 8.5* itakayokuwa na uwezo wa kuchinja *Ng'ombe 1,000* kwa siku hali itakayoondoa *uagizwaji wa Nyama Nje ya nchi* kwaajili ya kuuzwa kwenye *Hotel na Supermarket* ambapo kukamikika kwa mradi huu utawezesha *wazawa kupata soko la nyama la uhakika*, Ujenzi wa *Soko la Mburahati Billion Billion 2.7 kituo cha Daladala Tuangoma, Soko la Kibada Billion 14* pamoja na *miradi mingine mingi* ikiwemo *Fukwe za Coco, Ujenzi wa Shopping Mall* na miradi mingine lukuki inayofanywa na *Rais Magufuli* kwenye Mkoa wa Dar es salaam.
*RC Makonda* amemshukuru *Rais Magufuli* kwa kwa dhamira njema ya kusaidia *kutatua kero za wananchi* ambapo amewasihi wananchi wa Dar es salaam kukaa *mkao wa kula* kwa kuchangamkia *fursa za ajira* zitakazotolewa kwenye *miradi* hiyo.
*HUU NI UPENDO WA DHATI WA RAIS MAGUFULI KWA WANANCHI WAKE.*
Comments