KATIBU MKUU WIZARA YA HABARI AMTEMBELEA MWANARIADHA ANAYEHESHIMIKA DUNIANI MZEE JOHN STEVEN AKHWARI NYUMBANI KWAKE MBULU MKOANI MANYARA
Katibu
Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Suzan Mlawi
akisalimiana na Mzee John Steven Akhwari Mwanariadha anayeheshimika
Duniani mara baada kwasili alipomtembelea nyumbani kwake Eneo la Sani
mjini Mbulu mkoani Manyara jana, John Steven Akhwari aliiwakilisha nchi
katika michezo ya Olimpiki iliyofanyika Mexco City mwaka 1968
John
Steven Akwari aliyekuwa wa mwisho kumaliza mashindano ya marathon mwaka
1968 Mexico City katika mioyo ya mamilioni ya watu anakumbukwa kama
shujaa ambapo mwaka 2008 katika mashindano ya Olimpiki ya Beijing nchini
China miaka 40 baadaye, Akhwari aliteuliwa kuwa balozi wa heshima wa
Olimpiki. Katika mashindano hayo ya mwaka 1968, Akwari akiwa na umri wa
miaka 30 akiiwakilisha Tanzania alikuwa mwanariadha wa mwisho (57)
kumaliza mashindano kati ya 75 walioanza.
Mshindi
wa mashindano hayo Mamo Wolde wa Ethiopia alitumia saa 2:20:26 huku
Akhwari akimaliza zaidi ya saa moja baadaye yaani alitumia saa 3:25:27
kukiwa na watazamaji wachache uwanjani na jua lilikwisha kuzama. Awali
wakati anaanza mbio hizo, Akwari alianguka na kupata majeraha kwenye
goti ikichangiwa kwa kiasi kikubwa na hali ya hewa ya Amerika ya kati
kuwa tofauti na nyumbani. Wanariadha wenzake walimpita moja baada ya
mwingine na hivyo kukatiza ndoto yake ya kuiletea Tanzania medali ya
kwanza kabisa ya Olimpiki, lakini hakukata tamaa bali alinuia kumaliza
hayo mashindano.
Akiwa
amefungwa bandeji mguuni huku akitokwa na damu, Akhwari alitokeza
uwanjani saa moja baada ya mshindi kutangazwa, na kukiwa na watazamaji
wachache na waandishi wa habari na giza likianza kuingia, uwanja
ulizizima kuona Akhwari anachechemea akiwa na maumivu kuelekea mstari wa
kumaliza mbio, wengi waliguswa baada ya kushuhudia tukio hilo.
Alipoulizwa na waandishi kwa nini aliendelea na mashindano baada ya
kuumia, aliwajibu kwa utulivu jibu rahisi ``Nchi yangu haikunituma maili
zaidi ya 5000 kuanza mbio, bali kuzimaliza``
Mkurugenzi
wa Halmashauri ya Mbulu Bw. Hudson Kamoga akisalimiana na MZee John
Steven Akhwari wakati alipoongozana na Katibu Mkuu Wizara ya Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo aliyemtembelea mzee huyo nyumbani kwake eneo
la Sani mjini Mbulu.
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Suzan Mlawi akizungumza jambo na Mzee John Steven Akhwari.
Katibu
Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Suzan Mlawi
akimsikiliza Mee John Steven Akhwari alipokuwa aktoa maelezo kwake
kuhusu mbambo mbalimbali aliyowahi kuyafanya katika masuala ya mchezo wa
Riadha.
Katibu
Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Suzan Mlawi na
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu wakiangalia tuzo mbalimbali
ambazo Mzee John Steven Akhwari kulia aliwahi kutumikiwa.
Katibu
Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Suzan Mlawi na
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu wakionyeshwa mwenge wa
Olimpiki ambao Mzee John Steven Akhwari kulia kutumikiwa jijini Beijing
China baada ya kuukimbiza akiwa Balozi wa Mashindano hayo mwaka 2008.
Katibu
Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Suzan Mlawi
akionyeshwa moja ya tuzo ambayo Mzee John Steven Akhwari alitunukiwa
nchini Uswisi .
Katibu
Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Suzan Mlawi
akionyesswa Nisahani ambayo Mzee John Steven Akhwari alitunukiwa na Rais
Mstaafu wa awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi
Hapa
wakionyeshwa vyeti mbalimbali ambavyo Mzee John Steven Akhwari aliwahi
kutunikiwa kutambua mchango wake katika mchezo wa Riadha.
Katibu
Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Suzan Mlawi na
Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Mbulu Bw. Hudson Kamoga wakiwa
katika picha ya pamoja na Mzee John Steven Akhwari mara baada ya
mazungumza yao.
Comments