Man Utd ndiyo klabu yenye thamani kubwa zaidi Ulaya


Haki miliki ya picha Getty Images
Image caption Manchester United na Chelsea zote zimo kwenye 10 bora
Manchester United kwa mara nyingine wametangazwa kuwa klabu yenye thamani ya juu zaidi Ulaya, ambapo thamani yao inakadiriwa kuwa €3.25bn (£2.9bn) kwa mujibu wa kampuni ya KPMG.
Klabu hiyo ya England inaongoza kwa "thamani ya biashara", ikiwa mbele ya klabu nyingine kama vile Real Madrid na Barcelona.
Orodha hiyo imeandaliwa baada ya utafiti uliofanywa kwa kuangazia taarifa za kifedha za misimu ya 2015-16 na 2016-17 ambapo waliangazia faida, haki za utangazaji, umaarufu, matarajio kutokana na uwezo wa kimichezo na thamani ya uwanja.
Liverpool, ambao wamefika fainali Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya wamo nafasi ya nane kwenye orodha hiyo.
Kwenye utafiti huo ulioangazia klabu 32 kubwa, klabu za Ligi Kuu ya England zinajaza nafasi sita kati ya 10 za kwanza.
Andrea Sartori, mkuu wa michezo duniani katika KPMG ambaye ndiye mwandishi wa ripoti hiyo, anasema kwa jumla thamani ya klabu za soka imepanda katika mwaka uliopita.
"Ukuaji wa jumla unatokana na sababu kadha, moja ikiwa ni kuongezeka kwa mapato yanayotokana na uendeshaji shughuli katika klabu 32 kuu, ambao ulikuwa ni ukuaji 8%," alisema.
"Uhamisho wa wachezaji wa pesa nyingi pamoja na kuongezeka kwa mishahara hakujazuia klabu kuendelea kuongeza mapato, kwani faida kabla ya kutozwa ushuru uliongezeka kwa mara 17 ukilinganisha na mwaka uliotangulia."

Klabu 10 bora Ulaya kwa 'thamani ya biashara'
  • Manchester United - €3.255bn
  • Real Madrid - €2.92bn
  • Barcelona - €2.78bn
  • Bayern Munich - €2.55bn
  • Manchester City - €2.16bn
  • Arsenal - €2.10bn
  • Chelsea - €1.76bn
  • Liverpool - €1.58bn
  • Juventus - €1.30bn
  • Tottenham - €1.29bn
Chanzo: KPMG

Kando na kutawala orodha ya 10 bora, kulikuwa na klabu nyingine tatu za Uingereza katika orodha ya 20 bora - West Ham United, Leicester City na Everton.
SSC Napoli (nafasi ya 17) nao wamekuwa klabu ya pili kwa thamani Italia, nyuma ya Juventus lakini mbele ya AC na Inter Milan.
Mwaka huu, klabu 12 zilikuwa na thamani ya zaidi ya euro bilioni moja, mbili zaidi ya 2017 ambapo zilikuwaklabu kumi pekee.
Na klabu sita zina thamani ya zaidi ya euro bilioni mbili, tatu kutoka Ligi ya Premia, mbili kutoka Uhispania na moja ya Ujerumani.
Misimu ya 2015-16 na 2016-17, Manchester United walishinda Kombe la FA, Kombe la Ligi na Europa League. Lakini msimu huu wamemaliza bila kikombe hata kimoja.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*