MOI SASA KUFANYA UPASUAJI KWA WAGONJWA 1000 KWA MWEZI ASEMA MAKAMU WA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN.


NA WAMJW-DAR ES SALAAM

TAASISI ya Mifupa nchini MOI sasa itafanya upasuaji wa mifupa kwa wagonjwa wapatao 1000 kwa mwezi kutoka wagonjwa 500 mpaka 700 baada ya kupokea msaada wa chumba cha upasuaji na vifaa vyake kutoka kwa Serikali ya Kuwait .

Hayo yamesemwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan wakati wa kuzindua na kupokea msaada wa chumba cha upasuaji na vifaa vyake vyenye thamani ya shilinigi milioni 186 leo katika Taasisi ya mifupa MOI leo jijini Dar es salaam.

“Hii ni faraja kubwa sana kwa Serikali kwani uboreshwaji wa huduma katika hospitali zetu za kibingwa kubwa kama MOI itaweza kuhudumia wagonjwa wengi Zaidi kutoka wagonjwa 700 kwa mwezi mpaka kufikia 1000 kwa mwezi” alisema Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Aidha Makamu wa Rais Samia Suluhu amesema kuwa anaishukuru Serikali ya Kuwait kupitia Balozi wake Jasem Al Najem kwa msaada huo kwani utaisaidia kwa kiasi kikubwa MOI katika kuboresha utoaji huduma hasa katika fani ya upasuaji kwa watoto wenye vichwa vikubwa na mgongo wazi hapa nchini.

Kwa uapnde wake Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile amesema kuwa kukamilika kwa vyumba hivi viwili vya upasuaji, kutaiwezesha Taasisi ya MOI kuwa na jumla ya vyumba vya upasuaji 8 kutoka 6 vilivyopo sasa na miongoni mwa vyumba hivi vya upasuaji kimoja kitakuwa maalumu kwa ajili ya watoto tu.

“MOI imeshatoa matibabu ya upasuaji kwa wagonjwa 1,670 ikiwemo upasuaji mifupa (wagonjwa 1,228), kubadilisha nyonga (wagonjwa 84), kubadilisha goti (wagonjwa 72), upasuaji wa uti wa mgongo (wagonjwa 109), ubongo (wagonjwa 64), na watoto wenye vichwa vikubwa na mgongo wazi (wagonjwa 113” alisema Dkt. Ndugulile.

Aidha Dkt. Ndugulile amesema kuwa katika kuimarisha na kuboresha afya za Watanzania jengo hilo pia litakuwa na vitanda 16 vya ICU (Intensive Care Unit) na 16 vya HDU (High Dependency Unit), hivyo kuimarisha huduma za tiba kwa wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalumu.

Naye Balozi wa Kuwait Nchini Balozi Jasem Al Najem amesema kuwa Nchi ya Kuwait ipo mstari wa mbele katika kuhakikisha Hospitali na Vituo vya afya nchini Tanzania vinatoa huduma bora za Afya kwa kutumia Taaluma na ujuzi wa kisasa ikiwemo vifaa na vifaa tiba .

“Serikali ya Kuwait itakuwa mstari wa mbele katika kuunga mkono juhudi za Serikali ya Tanzania katika kuimarisha afya za wananchi kwa kuendelea kutoa misaada mbalimbali ikiwemo vifaa,vifaa tiba na wataalamu wa afya na kutochoka katika hilo” alisema Balozi Najem.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya MOI Bi. Zakia Mejhi amesema kuwa Taasisi yake imeokoa Bilioni 3 za kufanyia upasuaji kwani kwa sasa huduma hizo za kibingwa zinafanyika nchini kwa Shilingi Bilioni 12 kutoka Bilioni 15 za rufaa ya kwenda kutibiwa nje.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.