Mwanamume aliyeandamwa na nguruwe awaita polisi Marekani


A wild boar (file photo)Haki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Maafisa wa polisi hupokea simu zisizo za kawaida za watu wakiomba usaidizi, lakini kisa kimoja jimbo la Ohio kimewashangaza wengi. Polisi walipigiwa simu mapema Jumamosi na mwanamume aliyekuwa anahangaishwa na nguruwe.
Polisi walidhai pengine mwanamume huyo alikuwa anaota au alikuwa amelewa alipowaambia kwamba alikuwa anaandamwa na nguruwe akienda nyumbani.
"Tulifika kwa mwanamume huyo tuliyedhani alikuwa mlevi na kwamba alikuwa anaelekea nyumbani kutoka kwenye baa saa 11:26 asubuhi," polisi hao wanasema kwneye Facebook.
Lakini walipofika walimpata mwanamume alikuwa hajalewa hata kidogo, lakini hakufurahia kabisa kufuatwa na nguruwe.
Alikuwa anafutwa na nguruwe lakini hakujua afanye nini, polisi wa kituo cha Ridgeville Kaskazini wamesema.
Presentational white space
Polisi mmoja alifanikiwa kumkamata nguruwe huyo na kumuingiza kwenye gari la polisi na kumpiga picha.
Nguruwe huyo pia alipelekwa kwenye seli (chumba cha kuwafugia mbwa wa polisi) kabla ya kukabidhiwa kwa mmiliki wake Jumapili asubuhi.

Uliitazama hii?

Duma 'awajulia hali' watalii kwenye gari Tanzania

Mada zinazohusiana

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.