MAFUNZO YA UONGEZAJI THAMANI VIAZI LISHE YAFANA SUGECO

Washiriki wa Mafunzo ya Uongezaji Thamani Viazi Lishe kutoka mikoa mbalimbali nchini,wakionesha mikate na mandazi waliyotengeneza  kwa kutumia urojo wa viazi hivyo pamoja na unga wa ngano wakati wa mafunzo yaliyofanyika hivi karibuni katika Ushirika wa Wahitimu wa  Chuo Kikuu cha Kilimo Morogoro (Sugeco). Washiriki hao walifundishwa mambo mbalimbali ikiwemo uandaaji wa shamba, kupanda, uangalizi, mavuno, biashara pamoja na faida ya viazi hivyo vyenye  wingi wa vitamini A. Kushoto ni Mkurugenzi wa Sugeco, Revocatus Kimario.

Kuanzia leo naahidi kuwaletea yaliyojiri wakati wa mafunzo hayo yaliyoendeshwa na walimu makini na wenye weledi mkubwa  kuhusu zao hilo.MWANDAAJI RICHARD MWAIKENDA
Washiriki wakiosha viazi lishe ikiwa ni maandalizi ya awali

Wakimenya viazi lishe

wakiweka kwenye mashine ya kukata kata silesi tayari kwa kuanikwa kwenye mitambo ya kukausha inayotumia nishati ya jua.

Mshiriki Richard Mwaikenda ambaye kitaaluma ni mwandishi wa habari aliyeshiriki kwenye mafunzo hayo akisambaaza viazi vilivyokatwakatwa wakati wa kuvianika tayari kukaushwa kwenye mitambo inayotumia nishati ya jua.
Washiriki wakisambaza silesi za viazi lishe
Washiriki wakipata maelezo kutoka kwa Mtaalamu wa Viazi Lishe wa Sugeco, Jolenta Joseph
Washiriki wakipata maelezo kuhusu mfano wa kilimo cha umwagiliaji kinachotumi matone katika eneo la Segeco, Sua Morogoro.
Wakitembelea Dryer inayotumia Nishati ya jua
Richard Mwaikenda akiangalia aina ya mbegu ya viazi lishe  ya mataya katika bustani iliyopo Sugeco. Kushoto ni  Mtaalamu wa Viazi Lishe, Jolanta Joseph
Wakinywa Juisi iliyotengenezwa kwa kutumia viazi lishe. Kushoto ni Mkurugenzi wa Sugeco, Kimario na Mkufunzi wa Mafunzo ya Viazi Lishe, Massimba. Kulia ni wshiriki wa mafunzo hayo kutoka Dar. Doroth na Neema Ngowi.

Wakiwa kwenye mafunzo hayo
Viazi Lishe vilivyochemshwa kwa kutumia mvuke tayari kuwekwa kwenye mashine inayotengeza rojorojo inayotumika kutengenezea bidhaa mbalimbali
Washiriki wakijiandaa kuweka Viazi Lishe kwenye mashine ya rojorojo


Mashine ikitengeneza rojorojo inayotumika kwenye mandazi, mikate na bidhaa zinginezo
Mjasiriamali Nasra kutoka Dar es Salaam akipanga vizuri mikate baada ya kushiriki kuitengeneza
Mwalimu wa mafunzo hayo, Jolanta akitoa maelezo ya kuzingaatia wakati wa kutengez juisi
Washiriki wakikanda mchanganyiko wa unga wa ngano na viazi lishe tayari kutengeneza maandazi

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

ALLY KAMWE AZIMIA KWA MKAPA.

RAIS SAMIA KUZINDUA MKUTANO MKUU WA 79 WA BARAZA LA MICHEZO YA MAJESHI DUNIANI

MIGINGO KISIWA KIDOGO ZAIDI AFRIKA KILICHOGOMBEWA NA UGANDA, KENYA