Wauguzi na Wakunga 1220 wakila kiapo huku wakiwa wamewasha mishumaa ikiwa ni ishara ya kuwa na moyo wa upendo wanapotoa huduma kwa wagonjwa na wananchi kwa ujumla katika mahafali yaliyofanyika leo Desemba 8, 2021 jijini Dodoma.
Msajili wa Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania, Bi. Agnes Mtawa akiwasha mshumaa tayari kutumika kuwawashia wahitimu.
Watumishi wa Baraza la Uuguzi na Ukunga wakipiga makofi kwa furaha wakati wa mahafali.
Msajili wa Baraza, Bi. Mtawa akiwawashia mishumaa wahitimu.
Wahitimu wakiwashiana mishumaa.
Wahitimu wakiwa na mishumaa tayari kula kiapo.
Viongozi meza kuu wakiongoza kula kiapo
Mwenyekiti wa Baraza la Uuguzi na Ukunga, Profesa Lillian Mselle akihutubia wakati wa mahafali hayo.Mwenyekiti wa Baraza la Uuguzi na Ukunga, Profesa Lillian Mselle akiwakabidhi vyeti na leseni wahitimu.
Viongozi meza kuu wakiwa na baadhi ya wahitimu wa uuguzi na ukunga waliofanya vizuri katika mitihani na kukabidhiwa vyeti na leseni.
Baadhi ya wageni waalikwa wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi.
Watumishi wa Baraza wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi.
PICHA YOTE NA RICHARD MWAIKENDA
Mdau, nakuomba uendelee kusikiliza kupitia clip hii ya video, Mwenyekiti Profesa Mselle akihutubia, Msajili Bi. Mtawa akitoa shukrani na wahitimu wakielezea furaha yao baada ya kukabidhiwa vyeti na leseni .....
IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA 0754264203
Comments