Mwenyekiti mpya wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake ya Chama Cha Mapinduzi Tanzania (UWT), Mary Chatanda amesema kuwa maelekezo ya Mwenyekiti wa CCM, Rais Samia Suluhu Hassan aliyoyatoa alipokuwa akihutubia wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Kumi wa UWT Taifa, jijini Dodoma Novemba 28, 2022, ndiyo dira watakayoifanyia kazi.
Chatanda ametoa mwelekeo huo alipokuwa akihutubia wajumbe mara baada ya kutangazwa mshindi wa wadhifa huo na aliyekuwa msimamizi wa uchaguzi huo, Waziri Mkuu mstaafu, Mizengo Pinda kwenye Ukumbi wa Jakaya Kikwete.
PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA
Baadhi ya wajumbe kutoka mikoa mbalimbali nchini wakiwa kwenye mkutano huo mkuu wa uchaguzi.
Mdau, nakuomba uendelee kusikiliza kupitia clip hii ya video, Chatanda akitoa mwelekeo huo...
IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA
MSIMAMIZI MKUU
KAMANDA WA MATUKIO TV/BLOG
0754264203
Comments