Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Stephen Wasira, leo Mei 18, 2026, amefungua mafunzo yanayovishirikisha vyama sita vya kihistoria na ukombozi kutoka Kusini mwa Afrika, yakilenga kuimarisha mshikamano, uongozi thabiti, na misingi ya harakati za ukombozi barani Afrika.
Hafla ya ufunguzi imefanyika katika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere, Kibaha, taasisi ya pamoja inayomilikiwa na vyama hivyo vya ukombozi kwa ajili ya kujenga uwezo wa viongozi na kuendeleza ushirikiano wa kisiasa na kiitikadi.
Vyama vinavyoshiriki mafunzo hayo ni African National Congress (ANC) cha Afrika Kusini, Chama Cha Mapinduzi (CCM) cha Tanzania, FRELIMO cha Msumbiji, MPLA cha Angola, SWAPO cha Namibia, pamoja na ZANU-PF cha Zimbabwe.
Mafunzo hayo yanaendelea kuthibitisha dhamira ya vyama vya ukombozi kuimarisha ushirikiano wao wa kihistoria, kubadilishana uzoefu wa uongozi, na kuandaa kizazi kipya cha viongozi kitakachoendeleza ajenda ya maendeleo, umoja na ustawi wa wananchi wa Afrika. @frelimo_mocambique @officialzanupf @mplaoficial @ccmtanzania







Comments