ANGALIA PICHA WADADA HAWA WALIVYOPIGWA

 Akilia baada ya kula kichapo.
BALAA! Siku chache tu baada ya kumalizika kwa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan, warembo wawili ambao majina yao hayakufahamika haraka wamejikuta wakila kichapo kutoka kwa mabaunsa kufuatia kuchelewa kutoka ndani ya baa waliyokuwa wakipombeka. Tukio hilo la aina yake lilijiri Agosti 5, mwaka huu katika baa hiyo mpya iliyopo Sinza ya Afrikasana jijini Dar es Salaam.

 Ilidaiwa kuwa, warembo hao waliambiwa mapema kuwa ifikapo alfajiri wasionekane kwenye eneo la baa hiyo lakini wao waliendelea kupombeka  mpaka jua linachomoza ndipo mabaunsa walipowaondolea uvivu kwa kuwapa kipigo. Mmoja wa warembo hao ambaye alionekana kukerwa na kitendo cha mwenzake kupigwa hadi kutokwa damu aliwalalamikia mabaunsa hao kuwa hawajawatendea haki kwa kuwafukuza kama mbwa na kipigo juu
Akitokwa na damu juu ya jicho la upande wa kulia baada ya kuchezea kichapo kikali.

 Kwa vile hawakuwa na nguvu za kupigana na mabaunsa hao, warembo hao waliporomosha matusi ya nguoni na kujaza watu waliokuwa wakienda makazini asubuhi hiyo. 


Hata hivyo, baadhi ya mashuhuda waliokuwepo eneo la tukio, hasa wanaume walisikika wakipongeza kitendo cha warembo hao kuchezea kichapo wakisema wamezoea kukesha eneo hilo mpaka kunakucha.
Mashuhuda hao walikwenda mbele zaidi kwa kusema kuwa wanahisi warembo hao wanajihusisha na biashara ya ‘udada poa’.

Baadhi ya wananchi wakishuhudia mkasa huo.

 “He! Wamezoea hao! Ni sawa mabaunsa wawaoneshe kazi. Watu gani wapo baa hadi muda huu wa asubuhi kweupe?” alisikika mmoja wa mashuhuda hao. 


Kilio kikubwa cha mabaunsa hao kilikuwa ni kutaka kusimamia heshima ya baa hiyo kwa vile wateja wanaofika hapo ni wenye heshima zao. 

“Msije tena hapa, sisi hatuwataki muda wa asubuhi wala mchana, tulishasema sana lakini hamsikii, mnataka kutukimbizia wateja siyo?” alisema mmoja wa mabaunsa hao.

Wakishauliana jinsi ya kumsaidia mwenzao.

 Mwisho wa sakata hilo, warembo wengine walitafuta usafiri wa Bajaj na kumbeba mwenzao aliyepigwa sana mpaka kutoka manundu na kuondoka huku wakiendelea kuvurumisha mitusi kwa mabaunsa hao na kusema wanakwenda kutoa taarifa kwenye Kituo cha Polisi Kijitonyama ‘Mabatini’, Dar. 


Mapaparazi wetu waliifuatilia Bajaj hiyo na kuiona inaelekea maeneo ya Sinza ya Mapambano  badala ya polisi. 

Baadhi ya wateja wa baa hiyo walisema wakati wa Mfungo wa Ramadhan, warembo walipungua eneo la baa hiyo lakini sasa wamerudi tena ambapo sasa wanapatikana kuanzia saa moja jioni hadi jua linapochomoza kesho yake

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI