Mhe.
Balozi Dkt. Augustine Mahiga Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa
Afrika Mashariki, akisoma hotuba ya bajeti ya Wizara kwa mwaka wa fedha
2018/2019 bungeni jijini Dodoma.
Mapema
leo Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limepisha kiasi cha
Shilingi Bilioni Mia Moja Sabini na Saba, Milioni Sita na Mia Mbili
Thelathini na Mbili Elfu.
Kati
ya fedha hizo Shilingi Bilioni Mia Moja Sitini na Sita, Milioni Mia
Sita na Sita, na Mia Mbili Thelathini na Mbili Elfu ni kwa ajili ya
matumizi ya kawaida, na Shilingi Bilioni Kumi na Milioni Mia Nne ni kwa
ajili ya bajeti ya maendeleo.
Pro.
Adolf F. Mkenda Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa
Afrika Mashariki,(wa kwanza kushoto) akifuatilia uwasilishwaji wa hotuba
ya bajeti ya Wizara. Wa pili kutoka kushoto, ni Naibu Katibu Mkuu
Balozi Ramadhani Mwinyi akifuatilia hotuba.
Sehemu
ya Watendaji wa Wizara wakifuatilia hotuba ya bajeti ya Wizara kwa
mwaka wa fedha 2018/2019 iliyowasilishwa na kupishwa bungeni jijini
Dodoma .
Mhe.Balozi
Dkt. Augustine Mahiga akijibu maswali bungeni mara baada ya kuwasilisha
hotuba ya bajeti ya Wizara kwa mwaka wa fedha 2018/2019
Mhe.
Dkt. Susan Kolimba Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa
Afrika Mashariki (kushoto), akifuatilia hotuba ya bajeti bungeni jijini
Dodoma
Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akifafanua jambo mara baada ya kuwasilisha hotuba ya bajeti ya Wizara.
Mhe.
Balozi Dkt. Augustine Mahiga Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa
Afrika Mashariki, akisalimiana na Dkt. Stergomena Tax Katibu Mkuu wa
Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) walipokutana katika
viunga vya Bunge jijini Dodoma mara baada kuwasilisha hotuba ya bajeti
ya Wizara.
Mhe.
Waziri Mahiga akijadili jambo na Mhe. Zitto Kabwe Mbunge wa Kigoma
Mjini katika viunga vya Bunge jijini Dodoma mara baada ya kupitishwa kwa
hotuba ya bajeti ya Wizara
Mhe.
Waziri Mahiga na Mhe. Naibu Waziri Kolimba wakiwa katika picha ya
pamoja na baadhi ya Waheshimiwa Mabalozi na Watendaji wa Wizara
waliohudhuria tukio la uwasilishwaji wa bajeti ya Wizara bungeni jijini
Dodoma
HOTUBA YA MHESHIMIWA BALOZI DKT. AUGUSTINE PHILIP MAHIGA
(MB), WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI AKIWASILISHA
BUNGENI MAKADIRIO YA BAJETI YA MAPATO NA MATUMIZI YA WIZARA KWA MWAKA WA FEDHA
2018/2019
AF
|
Adaptation
Fund
|
AfDB
|
African Development Bank
|
AfCFTA
|
African Continental Free Trade
Area
|
AGOA
|
African Growth and Opportunity
Act
|
AICC
|
Arusha
International Conference Centre
|
AMISOM
|
African Union Mission to Somalia
|
APRM
|
African Peer Review Mechanism
|
BBC
|
British Broadcasting Corporation
|
CGTN
|
China Global Television Network
|
COMESA
|
Common Market for Eastern and
|
|
Southern Africa
|
COP
|
Conference of Parties
|
DW
|
Deutsche Welle
|
EAC
|
East African Community
|
EPA
|
Economic Partnership Agreement
|
FAO
|
Food and Agriculture
Organization
|
|
FIB
|
Force Intervention Brigade
|
|
FOCAC
|
Forum on China-Africa
Cooperation
|
|
ii
|
|
Green Climate Fund
|
|
GEF
|
Global Environment Facility
|
|
GIZ
|
The Deutsche Gesellschaft für
|
|
Internationale Zusammenarbeit
GmbH
|
|
|
|
GPEDC
|
Global Partnership for Effective
|
|
|
Development Cooperation
|
|
IAEA
|
International Atomic Energy
Agency
|
|
IGAD
|
Intergovernmental Authority on
|
|
|
Development
|
|
ILO
|
International Labour
Organization
|
|
IMF
|
International Monetary Fund
|
|
IOM
|
International
Organization for Migration
|
|
IORA
|
Indian Ocean Rim Association
|
|
JNICC
|
Julius
Nyerere International Convention
|
|
|
Centre
|
|
KCB
|
Kenya Commercial Bank
|
|
KOICA
|
Korea International Cooperation
Agency
|
|
LDCF
|
Least Developed Countries Fund
|
|
MINUSCA United Nations Multidimensional
Integrated
Stabilisation
Mission in the Central African Republic
MK-ICC Mt. Kilimanjaro International
Convention
Centre
MONUSCO United Nations Organisation
Stabilisation
Mission
in the Democratic Republic of the Congo
NPT Non – Proliferation Treaty
PSPF Public Sector Pension Fund
RFI Radio France International
RMB Renminbi
SADC Southern African Development
Community
SDGs Sustainable Development
Goals
TAZARA Tanzania-Zambia Railway Authority
TBC Tanzania Broadcasting Corporation
TEHAMA Teknolojia ya Habari na
Mawasiliano
TIC Tanzania Investment Centre
TMEA Trademark East Africa
UKIMWI Upungufu wa Kinga Mwilini
United
Nations African Union Mission in Darfur
UNDP
United Nations Development Progamme
UNDAP
United
Nations Development Assistance Plan
UNEP
United Nations Environment Progamme
UNESCO
United
Nations Educational Scientific and Cultural Organization
UNFPA
United Nations Population Fund
UN-HABITAT
United
Nations Human Settlement Programme
UNHCR
United
Nations High Commission for Refugees
UNICEF
United
Nations Children’s Emergency Fund
UN-ICTR
United
Nations International Criminal Tribunal for Rwanda
UNIDO
United
Nations Industrial Development Organization
UNIFIL
United Nations Interim Force in Lebanon
UNISFA
United
Nations Interim Security Force for Abyei
UNMISS United Nations Mission in the
Republic
of South Sudan
UTT Unit Trust of Tanzania
VoA Voice of America
WHO World Health Organization
WTO World Trade Organization
WWF World Wildlife Fund
1.
Mheshimiwa Spika, baada ya Mwenyekiti wa Kamati ya
Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kuwasilisha Taarifa ya
Utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Wizara, naomba sasa kutoa hoja kwamba Bunge
lako Tukufu likubali kupokea na kujadili taarifa ya utekelezaji wa mpango na
bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa mwaka
wa fedha 2017/18. Aidha, naomba Bunge lako Tukufu lijadili na kupitisha Mpango
na Bajeti ya Wizara kwa mwaka wa fedha 2018/19.
2.
Mheshimiwa Spika, awali ya yote napenda kumshukuru
Mwenyezi Mungu, mwingi wa fadhila na rehema, kwa
kutujalia afya njema na kutuwezesha kukutana tena katika Bunge lako Tukufu, kujadili Mpango na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya
Wizara yangu.
3.
Mheshimiwa Spika, naungana na wenzangu walionitangulia
kuwashukuru na kuwapongeza watoa hoja waliozungumza kabla yangu, hususan Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb), Waziri
Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; na Mheshimiwa Dkt. Philip Isdory
Mpango (Mb), Waziri wa Fedha na Mipango ambao kwa hakika hotuba zao sio tu
zimezungumzia mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Tano, bali pia zimetoa dira
katika mustakabali wa taifa letu kwa kuainisha masuala muhimu ya kitaifa,
kikanda na kimataifa ambayo baadhi yake yanagusa majukumu ya Wizara yangu.
4.
Mheshimiwa Spika, naomba pia nitumie fursa hii kutoa
shukrani zangu kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama
chini ya uongozi wa Mhe. Mussa Azan Zungu (Mb) na Makamu wake Mhe. Salum Mwinyi
Rehani (Mb). Kamati hii imetoa mchango mkubwa na imekuwa muhimili muhimu katika
kuiwezesha Wizara yangu kutekeleza majukumu yake kwa kutoa ushauri kuhusu
masuala mbalimbali ya kiutendaji.
5.
Mheshimiwa Spika, kwa namna ya pekee naomba nitumie
nafasi hii kuwashukuru Mheshimiwa Dkt. Susan Alphonce Kolimba (Mb), Naibu
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki; Prof. Adolf Faustine
Mkenda, Katibu Mkuu; Balozi Ramadhan Muombwa Mwinyi, Naibu Katibu Mkuu;
mabalozi wa Tanzania nje ya nchi; Wakuu wa Idara na Vitengo; watumishi wa
Wizara; na taasisi zilizo chini ya Wizara yangu kwa kujituma na kutekeleza
majukumu yao kwa weledi na kufanikisha kwa kiwango cha juu utekelezaji wa
bajeti ya mwaka wa fedha 2017/18, pamoja na kuandaa Bajeti ya Wizara ya mwaka
wa fedha 2018/19.
|
Comments