Taarifa kwa umma kuhusu kukamilika kwa zoezi la uteuzi wa

wagombea wa nafasi ya Spika

1.0 zoezi la Uteuzi wa Wagombea wa Uchaguzi wa Spika limekamilika

tarehe 10 Novemba, 2025 saa 10:00 Alasiri. Napenda kuchukua

nafasi hii kuwafahamisha yale yaliyotokana na zoezi hili na

mchakato mzima toka tulipoanza, tulipo na tunapoelekea.


2.0 Uchaguzi wa Spika unafanywa kwa mujibu wa lbara ya 86 (1) ya

Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977,

Kanuni ya 9 na Nyongeza ya Kwanza ya Kanuni za Kudumu za

Bunge, 2025.


3.0 ili kukidhi matakwa hayo, tarehe 4 Novemba, 2025 nilitoa Tangazo

namba 14824A katika Gazeti la Serikali Toleo Maalum Namba 11

kuvijulisha vyama vya siasa vyenye usajili w a kudumu

vinavyokusudia kusimamisha mgombea katika uchaguzi huo

Kufanya Mchakato na kuwasilisha jina la mgombea husika ofisini

kwa Katibu wa Bunge Dodoma kabla ya saa 10.00 jioni ya tarehe

10 Novemba, 2025 ambayo ndio siku ya uteuzi


4.0 Hadi kufikia saa 10:00 Alasiri leo tarehe 10 Novemba, 2025

Wagombea waliowasilishwa na Vyama vyao ni kama ifuatavyo:-

Mhe. Mussa Azzan Zungu kutoka Chama cha Mapinduzi

(CCM);

Ndg . Veronica Charles Tyeah kutoka Chama cha National

Reconstruction Alliance (NRA);

Ndg. Anitha Alfan Mgaya kutoka Chama cha National

League for Democracy (NLD):

Ndg Chrisant Nyakitita kutoka Chama cha Democratic Party

(DP)


Ndg. Ndonge Said Ndonge kutoka Chama cha Alliance for

Africa Farms Party (AAFP): na

Ndg. Amin Alfred Yango kutoka Chama cha Aliance for

Democratic Change (ADC).


5.0 Baada ya uchambuzi uliozingatia nafasi ya Kiti cha Spika, sifa za

wagombea waliopendekezwa na vyama na matakwa mengine ya

Kisheria na Kikanuni nimeridhika kwamba Wagombea wote

wametimiza masharti ya Kanuni

Uchaguzi. Hivyo,

za

nimewaidhinisha wagombea hao sita waliowasilishwa kwangu.


6. 0 Hivyo, bila kuathiri Shughuli nyingine zitakazopangwa na Bunge

tarehe 11 Novemba, 2025 saa Tatu asubuhi au muda mfupi baada

ya hapo, nitawasilisha majina ya Wagombea walioteuliwa kwa

Wapiga kura ambao ni Wabunge Wateule wa Bunge la Jamhuri ya

Muungano wa Tanzania ili Uchaguzi ufanyike kwa mujibu wa

utaratibu utakaotolewa wakati wa Uchaguzi

7.0 Napenda kutoa shukrani kwa Vyama vya Siasa vinavyohusika na

Wagombea wote kwa ushirikiano mlionipa katika kukamilisha zoezi

la Uteuzi.


Baraka I. Leonard


KATIBU WA BUNGE NA MSIMAMIZI WA UCHAGUZI

10 Novemba, 2025

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

VITU 10 WANAUME WANAVYOPENDA ZAIDI TOKA KWA MWANAMKE — SIYO SURA, SIYO MWILI ❤️

WALIOCHUKUA FOMU CCM ZA KUWANIA USPIKA HAWA HAPA

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

RAIS SAMIA SIO RAIS JOYCE BANDA WA MALAWI, TANZANIA SIO KENYA

MJUE VIZURI KOCHA MPYA WA YANGA PEDRO

MATOKEO YA DARASA LA 7 YATANGAZWA

JESHI LA POLISI LATEKELEZA AGIZO LA RAIS SAMIA, LAONDOA KIZUIZI CHA KUTOTOKA NJE BAADA YA SAA 12 JIONI