Msajiri wa Mahakama Rufaa Tanzania, Francis Mutungi (kushoto),Jaji Kiongozi, Fakih Jundu (kushoto), Jaji Mkuu wa Zanzibar, Hamid Mahamoud Hamid na Jaji wa Mahakama ya Rufani, Dk. Stephen Bwana (kulia) wakijadili jambo nje ya ukumbi wakati wakimsubiri Rais wa Zanzibar, Dk. Abeid Amani Karume kuwasili kwa ajili ya kufungua mkutano wa majaji wa nchi za Afrika Mashariki na Kati, kuhusu mapambano dhidi ya ugaidi katika ukanda huo na uhalifu wa kimataifa, jana uliofanyika jana katika hoteli ya Golden Tulip, Dar es Salaam
CHAMA KIPYA CHA WALIMU WAMUOMBA RAIS SAMIA AINGILE KATI MAKATO YA WANACHAMA WAO
Chama cha Kulinda na Kuwatetea Walimu Tanzania (CHAKUWAHATA) kimemuomba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kuingilia kati sakata la baadhi ya wakurugenzi kukiuka sheria ya kuwaruhusu walimu kujiunga na chama hicho hivyo makato ya fedha za mishahara yao kuingizwa kwenye chama hicho. Ombi hilo limetolewa na Mwenyekiti wa chama hicho, Emmanuel Herman alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari wakati wa Mkutano Mkuu wao unaofanyika jijini Dodoma. Walimu ambao ni wajumbe wa Mkutano Mkuu wa chama hicho wakiwa katika mkutano wa kupitia upya rasimu ya katiba ili ieendane na wakati.
Comments