Mmoja wa majeruhi akiwahishwa kupata tiba hospitali baada ya Gari la Abiria aina ya Toyota Hiace lenye namba za usajili T 373 BGT linalofanya safari zake katika barabara ya Moshi-Arusha, ambalo limesababisha ajali kwa kugongana na basi la Ngorika linalofanya safari za Arusha- Dar. Watu kumi walifariki katika ajali hiyo. (PICHA NA AMRI MVUNGI).
CHAMA KIPYA CHA WALIMU WAMUOMBA RAIS SAMIA AINGILE KATI MAKATO YA WANACHAMA WAO
Chama cha Kulinda na Kuwatetea Walimu Tanzania (CHAKUWAHATA) kimemuomba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kuingilia kati sakata la baadhi ya wakurugenzi kukiuka sheria ya kuwaruhusu walimu kujiunga na chama hicho hivyo makato ya fedha za mishahara yao kuingizwa kwenye chama hicho. Ombi hilo limetolewa na Mwenyekiti wa chama hicho, Emmanuel Herman alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari wakati wa Mkutano Mkuu wao unaofanyika jijini Dodoma. Walimu ambao ni wajumbe wa Mkutano Mkuu wa chama hicho wakiwa katika mkutano wa kupitia upya rasimu ya katiba ili ieendane na wakati.
Comments